×

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) yatangaza wajumbe wa viti maalum vya wanawake

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imetangaza majina ya wajumbe wa viti maalum vya wanawake watakaokuwemo katika Baraza la Wawakilishi, kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Thabit Aidarous, uteuzi huo umefanyika katika kikao maalum cha tume hiyo kilichofanyika tarehe 4 Novemba.

Jumla ya wajumbe 20 wa viti maalum wameteuliwa, wakiwemo wajumbe 16 kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) na wajumbe 4 kutoka Chama cha ACT-Wazalendo, kwa uwiano unaoakisi uwakilishi wa vyama hivyo katika Baraza la Wawakilishi.

Tume imesema uteuzi huo umefanywa kwa mujibu wa kifungu cha 67(1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, pamoja na kifungu cha 55(3) cha Sheria ya Uchaguzi Na. 4 ya mwaka 2018.

Haya yanajiri, baada ya Chama cha upinzani, ACT-Wazalendo, kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais visiwani Zanzibar.

Mgombea wa urais wa chama hicho Outhman Masoud alieleza kutoridhishwa kwake.

“Wananchi wa wameibiwa sauti yao… suluhu pekee ya kupata haki ni uchaguzi mpya,”

Leave a Comment