Vodacom Yagawa Makapu Ya Sikukuu Kwa Wateja Wake Mkoani Mbeya

Kampuni ya Vodacom Tanzania Plc imeendelea na zoezi lake la kugawa makapu ya sikukuu kwa wateja wake katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea msimu wa sikukuu na kutoa shukrani kwa uaminifu wa wateja.
Katika tukio lililofanyika eneo la Ipinda–Kyela jijini Mbeya, Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania Plc mkoa wa Iringa, Zidiel Mbwambo, alikabidhi Kapu la Sikukuu kwa Rehema Robert Mwang’onda kama ishara ya kuungana na wateja kusherehekea msimu huu wa furaha.

Aidha, Ofisa wa M-Pesa kutoka Vodacom Tanzania Plc, Evelyn Mwinuka, naye alikabidhi kapu jingine kwa mteja Lukas Njabeki Chuma, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kampuni hiyo ya kuwashukuru wateja wake kwa kuendelea kuitumia huduma za Vodacom na M-Pesa.
Zoezi hilo ni muendelezo wa mpango wa Vodacom Tanzania kugawa makapu ya sikukuu katika mikoa mbalimbali nchini, kama sehemu ya kuimarisha uhusiano na wateja na kusherehekea msimu wa sikukuu kwa pamoja.

