Yanga Yamtambulisha Mshambuliaji Laurindo Depu Kutoka Poland

Klabu ya Yanga rasmi imemtambulisha mshambuliaji wa kati Laurindo Dilson Maria Aurélio Depu (25), raia wa Angola, akitokea klabu ya Radomiak Radom ya Poland.
Depu amesaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia mabingwa hao wa Tanzania Bara, akitarajiwa kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji wa timu hiyo kuelekea mashindano ya ndani na kimataifa.
Usajili wa Depu ni sehemu ya mkakati wa Yanga kuendelea kuimarisha kikosi chake, hususan katika eneo la ushambuliaji, wakilenga mafanikio makubwa zaidi msimu ujao.

