The House of Social Media
gunners X

Rais Museveni atangazwa mshindi wa uchaguzi Uganda

0


Tume ya uchaguzi nchini Uganda imemtangaza Rais Yoweri Kaguta Museveni kama mshindi wa uchaguzi uliofanyika Alhamisi wiki hii, akiwa na jumla ya kura 7,946,772 ambayo ni asilimia 71.65% ya kura zote zilozopigwa.

Mpinzani wake wa karibu Robert Ssentamu Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine alikuwa wa pili, akiwa na jumla ya kura 2,741,238 au asilimia 24.72%.

Kwa mujibu wa tume hiyo, kura 11,366,201 zilipigwa katika uchaguzi huu wa mwaka 2026, ikiashiria asilimia 52.50% ya idadi ya wapiga kura waliojitokeza kushiriki.

Hata hivyo, kura 275,353 (2.42%) zilizopigwa zilikuwa batili.

Matokeo ya uchaguzi

Museveni 7,946,772 (71.65%)

Bobi Wine 2,741,238 (24.72%)

Bulira Frank 45,959 (0.41%)

Leave A Reply