×

TEMESA Yatangaza Nafasi 6 za Meneja wa Kanda, Maombi Mwisho Februari 20

Kwa niaba ya Wakala wa Huduma za Ufundi za Umeme, Mitambo na Elektroniki Tanzania (TEMESA), Ofisi ya Rais – Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) inakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa, weledi, uadilifu na ari ya kufanya kazi kujaza nafasi sita (6) za kazi kama ifuatavyo:


1. Nafasi: Meneja wa Kanda (Regional Manager) – Nafasi 6

Majukumu ya Kazi

  • Kusimamia uendeshaji wa shughuli za kanda kwa ufanisi na kuhakikisha huduma zinatolewa kwa wakati na kwa viwango vya ubora.

  • Kusimamia rasilimali za kazi zikiwemo vifaa, zana na mitambo bila kuzalisha gharama zisizo za lazima.

  • Kuboresha huduma kwa wateja kwa kuhakikisha malalamiko yanashughulikiwa haraka.

  • Kuongoza na kusimamia wasimamizi pamoja na wafanyakazi wa utawala.

  • Kuandaa na kusimamia bajeti ya kanda kwa kuzingatia matumizi yenye tija.

  • Kuratibu mafunzo kwa watumishi wa kiufundi ili kuongeza ujuzi.

  • Kushirikiana na timu za kiufundi kuboresha utoaji huduma.

  • Kutafuta fursa za kibiashara na kupanua wigo wa huduma za TEMESA ndani ya kanda husika.

  • Kujenga mahusiano mazuri na wadau, jamii na mamlaka za eneo.

  • Kuandaa taarifa za utendaji wa kanda mara kwa mara.

  • Kutekeleza majukumu mengine atakayopangiwa na msimamizi wake.


Sifa za Mwombaji

Mwombaji anatakiwa kuwa na:

  • Shahada ya Uzamili na Shahada ya Kwanza katika mojawapo ya fani zifuatazo:
    Biashara (Fedha/Marketing), Fedha, Uchumi, Takwimu, Utawala wa Umma, au Uhandisi (Umeme, Mitambo, Elektroniki, Electromechanical).

  • Waombaji wa Uhandisi lazima wawe wamesajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) kama Professional Engineer.

  • Uzoefu wa kazi usiopungua miaka 8 katika fani husika.

  • Shahada ya Uzamili inayohusiana na Shahada ya Kwanza ni faida zaidi.


Mshahara

TMSS 10


Masharti ya Jumla

  • Mwombaji awe raia wa Tanzania na asiwe na umri zaidi ya miaka 45.

  • Aambatanishe nakala zilizothibitishwa za vyeti vyote muhimu (elimu, taaluma, cheti cha kuzaliwa n.k).

  • Wasitumie result slips, testimonials au partial transcripts.

  • Aweke picha ya passport size ya hivi karibuni.

  • Waajiriwa wa Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba.

  • Aonyeshe majina ya wadhamini (referees) watatu.

  • Vyeti vya nje ya nchi vihalalishwe na TCU/NECTA/NACTVET.

Jinsi ya Kutuma Maombi

Maombi yote yawasilishwe kupitia Recruitment Portal ya PSRS pekee.

Mwisho wa Kutuma Maombi: 20 Februari, 2026

Katibu,
Ofisi ya Rais,
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma,
S.L.P 2320, Dodoma.

Leave a Comment