×

Video: Shigongo Akutana na Viongozi wa Usafirishaji, Afunguka Fursa za Mikopo Wezesha Mzawa

Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo na Mfanyabiashara maarufu nchini, Erick Shigongo.

Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo na Mfanyabiashara maarufu nchini, Erick Shigongo, amefanya mazungumzo na uongozi wa maafisa usafirishaji wa Mkoa wa Dar es Salaamuni ya Wezesha Mzawa, iliyopo Sinza Mori jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yalilenga kujadili maendeleo ya sekta ya usafirishaji, hususan changamoto na fursa zilizopo kwa madereva wa bodaboda na bajaji, pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya wadau wa sekta hiyo na taasisi za kifedha.

Akizungumza katika kikao hicho, Shigongo amesisitiza umuhimu wa kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji, akieleza kuwa uwepo wa mikopo na fursa za kifedha unaweza kusaidia kuboresha maisha ya wananchi wengi.

Kwa upande wao, uongozi wa maafisa usafirishaji wa Dar es Salaam wameishukuru kampuni ya Wezesha Mzawa kwa kutoa mikopo kwa wakati kwa madereva wa bodaboda na bajaji, jambo ambalo wamesema limechangia kwa kiasi kikubwa kuinua kipato na kuboresha huduma za usafiri jijini.

Wamesema msaada huo umesaidia kupunguza changamoto za mtaji kwa vijana wengi wanaojihusisha na sekta hiyo.

Leave a Comment