×

Trump Azua Gumzo Baada ya Kuchapisha Picha za AI Zenye Utata

Donald Trump ameibua mjadala mtandaoni baada ya kushirikisha picha kadhaa zilizotengenezwa kwa teknolojia ya Akili Unde (AI), ikiwemo moja inayomuonyesha akiwa kwenye noti ya dola 100 za Marekani.

Picha hizo alizichapisha kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, ambapo baadhi zilionyesha matukio ya kisiasa na kijeshi yenye utata mkubwa.

Moja ya picha hizo ilimuonyesha Trump akichukua nafasi ya Benjamin Franklin kwenye noti ya dola 100, huku noti hiyo ikipewa jina la “Federal Victory Note” badala ya “Federal Reserve Note.” Pia picha hiyo ilikuwa na maandishi kama “TRUMP2024” na “God Bless Donald Trump.”

Picha nyingine ziliwaonyesha viongozi wa Chama cha Democrats akiwemo Barack Obama, Joe Biden na Nancy Pelosi katika mazingira ya kejeli yaliyozua mjadala mkubwa mtandaoni.

Trump ameendelea kutumia mara kwa mara picha na maudhui ya AI kuwashambulia wapinzani wake wa kisiasa huku akiendeleza kampeni zake za kisiasa nchini Marekani.

MZEE LIPUTA MWENYE UPOFU na ANAYEMUUGUZA MKEWE APATA PIGO LINGINE – NYUMBA YOTE YADONDOKA…

Leave a Comment