Mama mmoja pamoja na mwanaye wanakabiliwa na tuhuma nzito za kumuua mtoto wa kambo katika tukio lililoibua simanzi na taharuki kubwa kwa wananchi, huku chanzo kikitajwa kuwa ni mgogoro wa mali za kifamilia.
Kwa mujibu wa taarifa za awali za uchunguzi, wawili hao wanadaiwa kupanga na kutekeleza tukio hilo baada ya kuzuka kwa mvutano wa muda mrefu kuhusu umiliki wa mali zilizokuwa zimeachwa na marehemu baba wa familia hiyo.