
Timu ya taifa ya England imetangaza rasmi namba za wachezaji wake kuelekea Kombe la Dunia 2026, hatua ambayo imeacha dalili kubwa kuhusu kikosi cha kwanza cha kocha Thomas Tuchel.
Kwa mujibu wa namba hizo, baadhi ya wachezaji wa kikosi hicho wamepewa namba zinazopendekeza nafasi zao za kucheza, jambo linaloashiria muundo wa kikosi kinachotarajiwa kuanza michezo yao ya mashindano.

Jordan Pickford ataendelea kuwa mlinda mlango namba 1, huku Harry Kane akipewa namba 9 kama mshambuliaji mkuu. Jude Bellingham amepata namba 10, Bukayo Saka namba 7, na Declan Rice namba 4.
Katika safu ya ulinzi, John Stones amepata namba 5 na Marc Guehi namba 6, huku Ezri Konsa akipewa namba 2 na Nico O’Reilly namba 3, jambo linalotoa ishara ya nafasi zao ndani ya mfumo wa timu.
Kwa upande wa washambuliaji, Marcus Rashford amevaa namba 11, huku Ollie Watkins akiwa namba 19 na Ivan Toney akichukua namba 22.

Orodha hiyo pia imejumuisha Kobbie Mainoo namba 16, Reece James namba 24 na wengine wengi, ikionyesha ushindani mkubwa ndani ya kikosi hicho cha wachezaji 26.
Mashabiki wa England sasa wanatafsiri namba hizo kama kidokezo cha kikosi cha kwanza cha Tuchel kitakachotumika kwenye michuano hiyo