
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amempokea Rais wa Jamhuri ya Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah aliyewasili nchini kwa ziara ya kitaifa leo Juni 20, 2026.
Hafla ya mapokezi imefanyika katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano kati ya Tanzania na Namibia.
Mapokezi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na ujumbe waandamizi kutoka pande zote mbili, ambapo nchi hizo zinatarajiwa kujadili na kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za maendeleo.




