Mji mkuu wa Venezuela Caracas, umekumbwa na matetemeko mawili makubwa yaliyoachana kwa sekunde chache.
Tetemeko la kwanza lilikuwa la ukubwa wa 7.2 lililotokea katika eneo la Montalbán, magharibi kidogo mwa Caracas, kulingana na shirika la ufuatiliaji wa Utafiti wa Jiolojia wa Marekani (USGC).
Sekunde 39 baadaye, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.5 lilipiga takriban kilomita 10 ndani ya eneo hilo.
Matetemeko hayo yametajwa kuwa moja ya mitetemeko mikubwa zaidi kuwahi kuikumba nchi hiyo ya Amerika Kusini katika karne moja.
Majengo yaliporomoka na wakaazi kukimbilia barabarani kutafuta usalama wakati matetemeko ya ardhi yalipotokea.
Rais wa mpito wa Venezeula Delcy Rodríguez ametangaza hali ya hatari.
Kuna hofu ya majeruhi na uharibifu mkubwa lakini hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusiana na hilo kufikia sasa. Waokoaji wako mbioni kuwatafuta manusura ambao huenda wamenaswa chini ya vifusi.