×

Maelfu Wafurika Mitaani Tehran Kuaga Mwili wa Ayatollah Ali Khamenei- (Picha +Video)

Msafara wa mazishi ya aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei,  leo Julai 6, 2026 umepitia mitaa ya mji mkuu wa Tehran, huku ukihudhuriwa na umati mkubwa wa waombolezaji waliokusanyika kutoa heshima zao za mwisho.

Khamenei, ambaye aliongoza Iran kwa zaidi ya miaka 35, aliuawa katika mashambulizi ya anga yaliyodaiwa kutekelezwa na Marekani na Israel mwezi Februari 2026.

Mazishi yake yalianza Ijumaa na yanatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku saba, yakijumuisha shughuli mbalimbali nchini Iran na Iraq.

Kwa mujibu wa mamlaka za Iran, kati ya watu milioni 12 na 20 wanatarajiwa kushiriki katika shughuli hizo za mazishi, jambo linaloifanya kuwa miongoni mwa hafla kubwa zaidi za kitaifa kuwahi kushuhudiwa nchini humo.

Wakati viongozi mbalimbali waandamizi wa utawala wa Iran wamejitokeza katika mazishi hayo, mrithi wa Khamenei, Mojtaba Khamenei, bado hajaonekana hadharani.

Kutokuwepo kwake kumezua uvumi kuhusu hali yake ya kiafya, kufuatia taarifa ambazo hazijathibitishwa zikidai kuwa alijeruhiwa katika mashambulizi hayo yaliyosababisha kifo cha baba yake. Mojtaba hajajitokeza hadharani tangu alipoteuliwa kushika nafasi ya uongozi mapema mwezi Machi.

Leave a Comment