×

Manchester United Yamtambulisha Karl Darlow Kwa Uhamisho Huru

Klabu ya Manchester United imethibitisha rasmi kumsajili kipa wa kimataifa wa Wales, Karl Darlow, kwa uhamisho huru akitokea Leeds United.

Darlow, mwenye umri wa miaka 35, amesaini mkataba wa miaka miwili utakaomuweka Old Trafford hadi Juni 2028, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi endapo pande zote zitakubaliana.

Usajili wa Darlow unakuja wakati hatma ya makipa André Onana na Altay Bayındır ikiendelea kuzua mjadala, huku wawili hao wakihusishwa na uwezekano wa kuondoka ndani ya dirisha hili la usajili.

Manchester United inaamini uzoefu mkubwa wa Darlow utakuwa msaada muhimu ndani ya kikosi, hasa katika idara ya makipa, ambapo anatarajiwa kuongeza ushindani na kuwa chaguo la kuaminika kwa benchi la ufundi msimu ujao.

Kipa huyo mwenye uzoefu mkubwa katika soka la England anajiunga na Mashetani Wekundu akiwa na matarajio ya kuchangia mafanikio ya klabu hiyo ndani na nje ya nchi.

Leave a Comment