×

Makamu wa Rais Nchimbi Ashiriki Misa ya Kumkumbuka Hayati Mkapa

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameungana na familia, waumini, viongozi mbalimbali pamoja na wananchi katika Misa Takatifu ya kumbukumbu ya miaka sita tangu kufariki kwa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameungana na Familia, Waumini, Viongozi na Wananchi mbalimbali katika Misa Takatifu ya kumbukumbu ya miaka sita tangu kufariki kwa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Benjamin William Mkapa, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Immaculate, Upanga Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 23 Julai 2026.

Ibada hiyo ilifanyika leo, Julai 23, 2026, katika Kanisa Katoliki la Parokia ya Mtakatifu Immaculate, Upanga, jijini Dar es Salaam, ambapo washiriki walipata nafasi ya kumuenzi na kumkumbuka Hayati Mkapa kwa mchango wake mkubwa katika uongozi na maendeleo ya Tanzania.

Misa hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa Serikali, viongozi wa dini, ndugu wa familia ya Hayati Mkapa pamoja na waumini na wananchi waliofika kutoa heshima zao kwa mmoja wa viongozi waliowahi kuliongoza taifa.

Makamu wa Rais, Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa pichani na wajane wawili (Anna Mkapa -Kushoto na Janeth Magufuli – Kulia)

Leave a Comment