×

Atletico Madrid Yakamilisha Usajili wa Lee Kang-in kutoka PSG

Klabu ya Atletico Madrid imetangaza kumsajili kiungo wa kimataifa wa Korea Kusini, Lee Kang-in, kutoka Paris Saint-Germain (PSG) kwa mkataba utakaodumu hadi Juni 2031.

Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, usajili huo unakadiriwa kugharimu hadi euro milioni 40.

Lee mwenye umri wa miaka 25 anarejea kucheza nchini Hispania baada ya kukaa misimu mitatu akiwa PSG, ambapo alicheza mechi 124, akifunga mabao 16 na kutoa pasi 16 za mabao.

Kabla ya kuhamia PSG mwaka 2023, Lee aliwahi kuichezea klabu za Valencia na Mallorca nchini Hispania.

Akiwa PSG, Lee alifanikiwa kutwaa mataji mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League), Kombe la UEFA Super Cup, Intercontinental Cup, mataji matatu ya Ligue 1, mataji mawili ya Coupe de France pamoja na mataji mawili ya French Super Cup.

Katika ngazi ya kimataifa, Lee alianza kuitumikia timu ya taifa ya Korea Kusini mwaka 2019 na tayari ameichezea mechi 50. Pia alikuwa sehemu ya kikosi cha taifa hilo katika Kombe la Dunia la mwaka 2022 na 2026.

Leave a Comment