×

Trump Atoa Taarifa Mpya Kuhusu Iran, Asema Hormuz Kufunguliwa Hivi Karibuni

Rais wa Marekani Donald Trump.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema serikali yake inaendelea kufanya mazungumzo mazuri sana na Iran, huku akieleza matumaini ya kufikiwa kwa makubaliano mapya.

Akizungumza katika kipindi cha Fox News, Trump alisema mazungumzo hayo yaliendelea kwa siku nzima jana, akisisitiza kuwa pande hizo zinafanya juhudi kutafuta suluhisho.

Trump pia amesema anaamini Mlango Bahari wa Hormuz utafunguliwa hivi karibuni, lakini akaonya kuwa Iran ikibadilisha msimamo wake tena inaweza kukabiliwa na hatua kali za kijeshi.

Kauli hiyo imekuja wakati masoko ya dunia yakionyesha matumaini ya kupungua kwa mvutano. Bei ya mafuta imeshuka huku masoko ya hisa nchini Marekani na Asia yakipanda kutokana na matarajio kuwa makubaliano yanaweza kufikiwa na shughuli za usafirishaji kupitia Hormuz kurejea kawaida.

Mlango Bahari wa Hormuz ni njia muhimu ya kimataifa kwa usafirishaji wa mafuta, hivyo hali ya usalama katika eneo hilo imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu na masoko ya dunia.

Leave a Comment