×

Karoline Leavitt Afichua Kazi Yake Mpya Baada ya Kujiuzulu White House

Karoline Leavitt, ambaye anatarajiwa kuondoka katika nafasi yake ya Msemaji wa Ikulu ya Marekani, White House Press Secretary.

WASHINGTON: Karoline Leavitt, ambaye anatarajiwa kuondoka katika nafasi yake ya Msemaji wa Ikulu ya Marekani, White House Press Secretary, amefichua kuwa ataendelea kufanya kazi kwa karibu na Rais Donald Trump baada ya kuondoka serikalini.

Leavitt amesema atarejea katika MAGA Inc. mwezi Septemba, ambako awali aliwahi kufanya kazi kabla ya kuwa msemaji wa kampeni ya Trump na baadaye kuteuliwa kuwa msemaji wa Ikulu.

Akizungumza na waandishi wa habari akiwa katika safari yake ya mwisho ndani ya ndege ya Rais Air Force One kuelekea kwenye mkutano wa Trump huko South Carolina Ijumaa, Agosti 21, Leavitt alisema atatumia muda kabla ya kurejea MAGA Inc. kuwa pamoja na familia yake.

Taarifa hiyo imekuja zaidi ya wiki moja baada ya Trump kutangaza kupitia mtandao wake wa Truth Social kuwa Leavitt ataondoka katika nafasi hiyo mwishoni mwa Agosti ili kutumia muda zaidi na watoto wake wadogo na familia.

Trump alisema Leavitt ataendelea kuwa mmoja wa washauri wake wakuu akiwa nje ya Ikulu na atakuwa na ushawishi ndani ya Chama cha Republican, hasa katika kuelekea uchaguzi wa katikati ya muhula.

Leavitt aliwahi kufanya kazi katika MAGA Inc. kabla ya kuwa msemaji wa kitaifa wa Trump na baadaye kushika nafasi ya White House Press Secretary.

Pia amerejea kazini hivi karibuni baada ya likizo ya uzazi. Yeye na mume wake, Nicholas Riccio, walipata mtoto wao wa pili mwezi Mei.

Kwa kurejea kwake MAGA Inc., Leavitt anatarajiwa kuendelea kuwa sehemu muhimu ya timu inayomsaidia Trump kisiasa, hususan katika maandalizi ya uchaguzi wa katikati ya muhula wa Marekani.

Leave a Comment