×

Mama Wa Miaka 18 Ashtakiwa kwa Mauaji Ya Mtoto Wake Wa Miaka Miwili

Mwanamke mwenye umri wa miaka 18, Devorah Diaz Perez.

Mwanamke mwenye umri wa miaka 18, Devorah Diaz Perez, amekamatwa na kushtakiwa kwa mauaji ya mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka miwili, katika jimbo la Georgia nchini Marekani.

Kukamatwa kwake kumekuja zaidi ya wiki mbili baada ya mpenzi wake wa kuishi naye, Celso Edison Vicente Y Vicente, mwenye umri wa miaka 22, kukamatwa na kushtakiwa kwa mauaji ya kukusudia pamoja na ukatili wa kiwango cha kwanza dhidi ya mtoto huyo.

Kwa mujibu wa Polisi wa Canton, tukio hilo lilianza kuchunguzwa Agosti 3, 2026, baada ya polisi kupokea taarifa ya mtoto mwenye umri wa miaka miwili kutokuwa na fahamu katika nyumba iliyopo eneo la Cartersville Street.

Celso Edison Vicente Y Vicente, mwenye umri wa miaka 22 mpenzi wake na Devorah Diaz Perez.

Mtoto huyo alipelekwa hospitalini kwa matibabu, lakini baadaye alitangazwa kuwa amefariki. Uchunguzi wa polisi uliendelea na kumhusisha Vicente Y Vicente, ambaye alidaiwa kuwa anahusika na kumtunza mtoto huyo siku ya tukio.

Hati za mashtaka zinadai kuwa Vicente Y Vicente alimpiga mtoto huyo kwa mikono na vitu vingine ambavyo havijafahamika, huku mtoto huyo akidaiwa kuwa na michubuko mingi mwilini, ikiwemo alama iliyofanana na chapa ya kiatu, pamoja na jeraha lililokuwa wazi kichwani.

Baada ya uchunguzi zaidi, polisi walimkamata pia mama wa mtoto huyo na kumshtaki kwa mauaji ya daraja la pili, makosa mawili ya ukatili dhidi ya watoto.

Polisi wamesema uchunguzi bado unaendelea na hawajatoa maelezo zaidi kuhusu ushahidi au mazingira ya kifo hicho kwa sababu kesi bado iko katika hatua za kisheria.

Ofisi ya Mchunguzi wa Kimatibabu ya Georgia Bureau of Investigation inatarajiwa kufanya uchunguzi wa mwili wa mtoto huyo ili kubaini rasmi chanzo na namna ya kifo chake.

Polisi wa Canton wamesisitiza kuwa watu wote wanaoshtakiwa wanachukuliwa kuwa hawana hatia hadi pale watakapothibitishwa kuwa na hatia na mahakama.

Leave a Comment