Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, amelipongeza Kanisa Katoliki kwa mchango wake katika kuhubiri amani na utulivu nchini Tanzania.
Shigongo ametoa kauli hiyo wakati wa Jubilee ya Miaka 25 ya Upadri ya Padre Cleophace Magesa, iliyofanyika nyumbani kwao katika Kigango cha Itulabusiga, Parokia ya Mwangia ya Mwangika.
Amesema madhehebu mbalimbali ya dini yamekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha amani nchini, akisisitiza kuwa amani ni msingi muhimu wa maisha ya jamii.
“Hivyo, tuendelee kuwaombea viongozi wa dini kwa kazi waliyonayo ya kuhubiri amani na utulivu ndani ya nchi yetu,” amesema Shigongo.
Aidha, Shigongo amesema juhudi za viongozi wa dini katika kuhubiri amani zinapaswa kuthaminiwa na kuungwa mkono kutokana na nafasi yao katika kujenga jamii yenye mshikamano na utulivu.