×

Allen Robinson Astaafu NFL Baada ya Miaka 11, Aanza Maisha Mpya

Mchezaji wa zamani wa Ligi ya Soka ya Marekani (NFL), Allen Robinson, ametangaza kustaafu kucheza soka la Marekani akiwa na umri wa miaka 33, baada ya kutumia miaka 11 katika ligi hiyo.

Robinson alitangaza uamuzi huo Jumatatu, Agosti 24, kupitia ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram, akiambatanisha video iliyosimulia safari yake ya kimichezo.

Robinson alianza kucheza NFL mwaka 2014 baada ya kuchaguliwa na Jacksonville Jaguars. Mwaka wake wa pili katika ligi ulikuwa wa kipekee kwake baada ya kuongoza ligi kwa kufunga touchdown 14 na kukusanya yadi 1,400, kiwango kilichomuwezesha kuchaguliwa katika Pro Bowl yake pekee.

Baada ya kuondoka Jacksonville Jaguars, Robinson aliwahi kuichezea Chicago Bears, Los Angeles Rams, Pittsburgh Steelers na Detroit Lions.

Mchezo wake wa mwisho katika NFL ulikuwa mwaka 2024 akiwa na Detroit Lions, huku akiwa hakushiriki msimu wa 2025.

Katika kipindi chake cha miaka 11 katika NFL, Robinson alimaliza akiwa na jumla ya receptions 565, receiving yards 7,058 na touchdown 43.

Robinson amesema sasa anaanza sura mpya ya maisha yake, huku akieleza shukrani kwa safari yake ya soka, pamoja na watu mbalimbali aliokutana nao na waliomsaidia katika kipindi chote cha maisha yake ya kimichezo.

Uamuzi huo unahitimisha safari ya miaka 11 ya Robinson katika NFL, ambapo aliibuka miongoni mwa wapokeaji muhimu wa pasi katika baadhi ya misimu ya ligi hiyo.

Leave a Comment