×

Kesi ya Uhaini: Lissu Akabiliana na Maswali ya Upande wa Jamhuri

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ameanza kukabiliana na maswali ya upande wa Jamhuri baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake mkuu katika kesi ya uhaini inayomkabili.

Dodoso hilo limeanza baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, kuahirisha mwenendo wa kesi kwa muda wa saa moja na nusu baada ya Lissu kukamilisha ushahidi wake wa msingi.

Mawakili wa upande wa Jamhuri, wakiongozwa katika hatua hiyo na Nassoro Katuga, wameanza kumuuliza Lissu maswali mbalimbali yanayohusu ushahidi alioutoa mbele ya jopo la majaji watatu.

Mwanzoni mwa dodoso hilo, Katuga alimpongeza Lissu kwa ushahidi mrefu alioutoa kabla ya kumtaka athibitishe kuwa anafahamu kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mchakato wa kisheria.

Lissu alikubaliana na kauli hiyo, akisisitiza kuwa yeye ni wakili wa Mahakama Kuu na ana uelewa wa sheria.

Nassoro Katuga: Shahidi pole na ushahidi mrefu

Lissu: Ahsante sana

Katuga: Kama nimekusikia vyema ulisema utatuacha sisi ndugu zako tukuulize maswali.

Lissu: Sahihi.

Katuga: Waambie majaji hiki tunachokifanya ni kitu cha kisheria na hakina nasaba nyingine yeyote.

Katuga: Uliiambia mahakama wewe ni wakili wa mahakama kuu na una ujuzi wa kisheria.

Lissu: Ndio

Katuga: Hebu waambie majaji Tanzania ilipata uhuru mwaka gani.

Lissu: 9/12/1961

Katuga: Kwa majibu hayo Tanzania ni nchi huru.

Lissu: Ndio

Katuga: Chombo cha mwisho cha kufanya maamuzi ya mwisho kwa mujibu wa kisheria ni ni kipi?

Lissu: Mahakama

Katuga: Mahakama haitakiwi kuingiliwa na mtu yeyote inapotoa maamuzi na pia mahakama hailazimishwi wala haipingwi na mtu au chombo chochote toka nje au ndani.

Lissu: Sahihi haipangiwi walakulazimishwa.

Katuga: Umetuambia wewe ni Mwenyekiti wa Chadema, Je katika utetezi wako umeimbia mahakama hii kuwa mwenyekiti wa Chadema ana kinga?

Lissu; Hapana na sina kinga hiyo

Katuga: Ndugu shahidi kama nilikupata vyema ulieleza sifa nyingi kukuhusu wala sizikatai iambie mahakama hizi tuzo ulizopewa ziko kwenye form gani kama maandishi au katika hali gani.

Lissu: Ziko katika hali ya maandishi, na ile alama yenyewe

Katuga: Ka object flani hivi.

Lissu: Ndio

Katuga: Embu iambie haya matuzo yote haya umeyaleta mahakamani

Lissu: Hapana na sina sababu ya kuyaleta.

Katuga: Twende pole pole tutakuwa na siku saba hapa.

Lissu: Hakuna neno

Katuga: Wewe umeleta nini hapa

Lissu: Maneno

Katuga: Sasa wewe uliposema mashahidi wa jamuhuri wameleta meneno ulimaanisha nini?

Lissu: Siwajibiki kufanya hivyo mimi nimeleta maneno sababu sina kesi ya kuthibitisha

Katuga: Sheria inasemaje?

Lissu: Sheria inataka mtu alete ushahidi pamoja na vithibitisho

Katuga: Unajua usilete ujuaji

Lissu: Yes mimi mjuaji

Katuga: Principles gani zinakutaka ulete maneno bila vithibitisho?

Lissu: Mimi sina wajibu wa kuthibitisha lolote.

Katuga: Unajua kifungu cha sheria kinasema yule anasema ana wajihi fulani anapaswa kuthibitisha.

Lissu: Ndio ninathibitisha

Katuga: Ulisema mahakama ni chombo huru wale uliosema wameelekeza uachiwe na unakubali mahakama ni chombo huru ndani ya nchi huru ya Tanzania?

Lissu: Ndio, Kamati ya haki za binadamu ya Umpja wa Mataifa

Katuga: Shahidi kuna mahali popote kwenye ushahdi wako kuna umekanusha maneno haya ya tunakwenda kukinukisha kweli kweli?

Lissu: Nimesema hivi maneno hayo ukitaka kuyaelewa unabidi usikilize hotuba yote.

Katuga: Mimi siwezi kukuuliza una akili timamu wewe ni kaka yangu

Lissu: Niulize tu

Katuga: Siwezi swali langu kuna mahali umekanusha maneno haya

Lissu: Hapana

Katuga: Kwa maana hiyo maneno haya huyakatai

Lissu: Siyakatai wala hayana shida.

Katuga: Nilitaka tu hicho

Lissu: Nimesema mara kadhaa.

Leave a Comment