×

Mashabiki, Wasanii Wamwaga Pongezi Kwa Maua Sama Baada Ya Picha Za Ujauzito

Msanii wa muziki wa Tanzania, Maua Sama, amezua furaha miongoni mwa mashabiki na mastaa mbalimbali baada ya kushiriki picha na video zinazomuonesha akiwa na ujauzito.

Maua Sama alishiriki picha na video hizo kupitia mitandao yake ya kijamii na kuandika ujumbe mfupi wa shukrani akisema, “I’m Grateful Alhamdulillah ❤️.”

Baada ya chapisho hilo, sehemu ya mastaa mbalimbali waliingia kwenye maoni na kumpongeza msanii huyo kwa hatua hiyo mpya ya maisha.

Msanii Jux aliandika, “Hongera sana,” huku Chege akisema, “Baraka za kutosha 🙏.”

Kwa upande wake, Dayana Nyange alionesha furaha kubwa na kumuandikia Maua Sama ujumbe wa pongezi akisema:

“Awwwww Kifua nnacho boo 😍😍😍 Anti Nimeweaza👌 Jamaniii hongera sasa Mama kijacho @mauasama Im so Happy for you love🥰❤️🫶.”

Naye Mamama Chanja alionesha mshangao na furaha kupitia ujumbe wake uliosomeka, “WOOOOOOOOOOOOOOOOOOW NIMESHAUTI HAPA JAMANI 🥹🙏🏻🙏🏻🙏🏻.”

Msanii Ammygal pia hakusita kumpongeza Maua Sama kwa kuandika, “Aaaaaaaw😍😍 Congrats Samaaa wangu😍.”

Aidha, Kim Nana alijiunga na mastaa hao kwa kumpongeza Maua Sama na kusema, “Hongera Babe👏👏😍😍.”

Pongezi hizo zimeendelea kuonyesha namna habari hiyo ilivyopokelewa kwa furaha na watu mbalimbali, huku mashabiki wakimtakia Maua Sama safari njema katika hatua hiyo mpya ya maisha.

Leave a Comment