×

Friji Bovu: Libasse Gueye Mmoja ni Sawa na Mawinga Wote – Video

Mchambuzi wa soka, David Pascol, maarufu kama ‘Friji Bovu’.

Mchambuzi wa soka, David Pascol, maarufu kama ‘Friji Bovu’, amesema atashangaa endapo kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Libasse Gueye, hatashinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi kutokana na kiwango alichoonyesha katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara mwezi huu.

Akizungumza kupitia Global TV, Pascol amesema Libasse ni mchezaji bora na ameonyesha uwezo mkubwa ndani ya uwanja, huku akitoa kauli kali kwamba:
“Libasse Gueye mmoja ni sawa na mawinga wote wa Ligi Kuu Tanzania Bara.”

Kauli hiyo ameitoa alipofanyiwa mahojiano na mtangazaji wa Global TV, @officialcosmo_, huku akisisitiza ubora wa mshambuliaji huyo wa Simba katika kipindi hiki.

Leave a Comment