×

Golugwa Aieleza Mahakama Juu Ya Ushiriki Wa Lissu Kwenye Mkutano

SHAHIDI WA TATU wa upande wa utetezi katika kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, Aman Sam Golugwa (Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA) leo Septemba 4, 2026 ameieleza Mahakama kuhusu mazingira ya mkutano wa chama uliofanyika Aprili 3, 2025, pamoja na madai mbalimbali yanayohusiana na kesi hiyo.

Akihojiwa na mawakili, Golugwa amesema Lissu hakushiriki katika maandalizi ya mkutano huo, ikiwa ni pamoja na kuwaita watia nia au kuwaalika waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa shahidi huyo, wakati maandalizi ya mkutano huo yakifanyika, Lissu alikuwa katika Operesheni ya CHADEMA iliyokuwa ikiendelea Kanda ya Nyasa yenye kaulimbiu ya “No Reforms, No Elections”.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Aman Sam Golugwa.

Golugwa amesema yeye mwenyewe aliwasiliana kwa simu na baadhi ya viongozi wakuu wa chama, akiwemo Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti Bara John Heche, Makamu Mwenyekiti Zanzibar Said Mzee Saidi pamoja na Naibu Katibu Mkuu, kuwaeleza kuhusu uwepo wa mkutano huo.

Amesema waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo walialikwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia, ambaye pia ni mjumbe wa Sekretarieti.

Shahidi ameitajia Mahakama baadhi ya vyombo vya habari alivyokumbuka kuwepo katika mkutano huo kuwa ni Clouds TV, Jambo TV, Chanzo TV, ITV na Gazeti la Mwananchi.

Golugwa amesema hakukuwa na masharti maalumu wala maelekezo yaliyotolewa kwa waandishi wa habari kuhusu namna ya kutekeleza majukumu yao katika mkutano huo.

Pia amesema kulikuwa na matangazo ya moja kwa moja kutoka katika mkutano huo, akivitaja Jambo TV na Chanzo TV kuwa miongoni mwa vyombo vilivyorusha matangazo hayo.

Kuhusu madai kwamba Tundu Lissu ndiye aliyerushaa matangazo hayo kupitia Jambo TV, Golugwa amekanusha na kusema madai hayo ni “uongo na upotoshaji”.

Aidha, amesema maneno yaliyochapishwa na Jambo TV yalichapishwa na mwandishi wa habari wa chombo hicho aliyekuwa amealikwa katika mkutano huo, na kwamba Lissu hakuhusika katika kuyachapisha.

GOLUGWA: HAKUKUWA NA MANENO YA KUCHOMA VITUO

Katika sehemu nyingine ya ushahidi wake, Golugwa amekanusha kuwepo kwa maneno yaliyodaiwa kuhusu kuchoma vituo vya mwendokasi au vituo vya kupigia kura.

Akiulizwa kuhusu maneno aliyosomewa mahakamani, shahidi amesema hakuna sehemu aliyosikia ikisema “tutachoma vituo vya mwendokasi” wala “tutachoma vituo vya kupigia kura”.

Pia amesema katika maneno hayo hakukuwa na kauli inayomtaja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

RIPOTI ZA WAANGALIZI

Golugwa pia amehojiwa kuhusu ripoti za waangalizi wa uchaguzi alizozitaja katika ushahidi wake.

Amesema ripoti hizo ni za mwaka uliopita na kwamba yeye alizitafuta na kuzihifadhi, lakini hakuzifikisha mahakamani.

Ameeleza kuwa ripoti hizo zimeandikwa kwa lugha ya Kiingereza na kukiri kuwa yeye si mwandishi wa ripoti hizo.

Katika mahojiano hayo, shahidi amesema hana elimu ya sheria, lakini amedai kuwa hata mtu asiye na utaalamu wa sheria anaweza kuzungumza mbele ya mahakama.

Kuhusu uwezo wake wa kutafsiri ripoti kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili, Golugwa amesema tafsiri isiyo sahihi inaweza kuathiri maana ya ripoti, ingawa amesema si lazima kueleza kiwango chake cha ufaulu wa Kiingereza.

GOLUGWA AKANUSHA KUWA NA IMANI NA RIPOTI NZIMA YA JAJI CHANDE

Katika sehemu nyingine, shahidi amesema hana imani na ripoti yote ya Jaji Chande, lakini amesisitiza kuwa baadhi ya mambo aliyoyazungumza mahakamani yana msingi katika kile alichokielewa mwenyewe.

Ameeleza pia kuwa hakumbuki baadhi ya taarifa zilizohusiana na ripoti za waangalizi, ikiwemo majina au vichwa vya baadhi ya ripoti alizoulizwa.

MALALAMIKO YA UCHAGUZI

Golugwa ameiambia Mahakama kuwa hakuwahi kujaza wala kuwasilisha fomu za kugombea nafasi yoyote katika uchaguzi huo.

Amesema malalamiko aliyoyazungumza mahakamani yalihusu wagombea na kwamba malalamiko hayo yaliwasilishwa katika mamlaka husika pamoja na kamati za rufaa.

Alipoulizwa kama malalamiko hayo yalipelekwa mahakamani baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya kamati za rufaa, Golugwa amesema hawakuona haja ya kwenda mahakamani kwa sababu, kwa mtazamo wao, “mambo ya kisiasa tunamaliza kisiasa”.

GOLUGWA: WATAZAMAJI WA KIMATAIFA WALIPINGA KESI YA UHAINI

Katika ushahidi wake kuhusu kesi inayomkabili Lissu, Golugwa amesema baadhi ya watazamaji wa kimataifa walionyesha masikitiko kuhusu kufunguliwa kwa kesi hiyo.

Kwa mujibu wa ushahidi wake, watazamaji hao walidai kuwa hawakuona mazingira ya uhaini katika maneno yaliyotajwa kuwa yalizungumzwa na Lissu na walitaka aachiliwe bila masharti.

Pia amesema Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lilieleza kuwa kukamatwa kwa Lissu hakukuwa halali na kwamba shtaka dhidi yake lilikuwa na lengo la kumuumiza kisiasa.

Golugwa pia amedai kuwa kikao cha Mawaziri wa Jumuiya ya Madola kilieleza kuwa kesi hiyo ilikuwa ya kisiasa na kuitaka Lissu aachiliwe bila masharti.

SABABU ZA VIFO NA MAUAJI

Akijibu swali kuhusu sababu zilizotolewa na Jaji Mkuu kuhusiana na mauaji yaliyotokea, Golugwa amesema kwa kumbukumbu zake sababu hizo zilihusisha madai ya Katiba Mpya, masuala ya utekaji na watu kupotea pamoja na manung’uniko ya muda mrefu ya wananchi ambayo hayakuwa yametatuliwa.

Ushahidi wa Golugwa unaendelea katika Mahakama, huku upande wa utetezi ukiendelea kumuuliza maswali kuhusu mkutano wa Aprili 3, 2025, maandalizi yake, ushiriki wa Lissu na maudhui ya maneno yanayohusishwa na kesi hiyo.

Ignas: Nimesikia ulikuwa kampeni meneja na hukugombea nafasi yoyote ile

Golugwa: Ni kweli

Ignas: Kwa hiyo ulipata hizo taarifa kwa watu wengine

Golugwa: Kwa kuwa nilikuwa karibu na wagombea nilikua naona kila kitu

Iganas: Unatambua matokeo ya uchaguzi ngazi ya ubunge 2020 yanapingwa mahakamani na yapi mlishinda

Golugwa: Kama nilivyosema chaguzi hizi siwezi kukumbuka ni malalamiko mangapi

Ignas: Je jambo lolote ambalo mliwasilisha mahakamani na mahakama ikaona hoja zenu zina msingi

Golugwa; Sikumbuki

Ignas: Unaweza sasa kuiambia hapa kuwa hoja ulizoleta hapa mahakamani hazikuwa na msingi na hivyo zipuuzwe

Golugwa: Hapana ni hoja za msingi

Ignas: Kwa kuwa umelamikia swala la madiwani embu tuambie ni kata ngapi malalamiko yenu yalithibitisha ni sahihi

Golugwa: Kwenye ngazi ya mahakama sina idadi

Ignas: Utakubaliana nami malalamiko yenu hayakuthibitishwa na mahakama?

Golugwa: Sio kweli yalikuwa ni ya kweli

Ignas: Ni mashauri mangapi mliwasilisha mahakamani

Golugwa: Hakuna

Ignas: Mahakamani hamkupeleka

Golugwa: Uchaguzi ni swala la kisiasa

Ignas: Hebu tuambie ya kwamba ni maneno ya kusikia na kamati za rufaa zilikubali malamiko yao yalikuwa na shida

Golugwa: Yote yalitupiliwa mbali

Ignas: Sababu hayakuwa na mashiko

Golugwa: yalitupiliwa mbali sababu ya uhuni na ushenzi

Mambo ya kisiasa tunamaliza kisiasa – Golugwa

Maswali ya Dodoso kwa shahidi namba tatu Aman Sam Golugwa

Ignas: Ni kweli hukujaza wala kuwasilisha fomu za kugombea katika mamlaka husika

Golugwa: Sikujaza fomu yoyote ya kugombea

Ignas: Ni kweli kwamba hukuwasilisha fomu

Golugwa: Ni kweli

Ignas: Ni kweli kwamba malamiko uliyoleta hapa mahakamani yalikuwa yanahusu wagombea

Golugwa: Ni kweli

Ignas: Malamiko uliyosema hapa mahakamani umeyapata toka vyanzo vingine

Golugwa: Sio kweli

Ignas: Mtu akiwa na malalamiko anapeleka wapi

Golugwa: Kwenye mamlaka husika

Iganas: Inamaana hujui wapi malamiko yanapopelekwa

Golugwa: Anapaswa kupelekea pale anapogombea na kwenye kamati ya rufaa

Ignas: Mlishinda mangapi

Golugwa: Yalitupiwa mbali sababu ya ushenzi niliosema

Ignas: Mliwasilisha hayo malalamiko yenu mahakamani

Golugwa: Tuna tambua ila hatukuona haja ya kwenda mahakamani

Ignas: Inamaana mlirudhika na maamuzi ya kamati za rufa:

Golugwa: Hapana mambo ya kisiasa tunamaliza kisiasa

Ignas: Kwenye zile kanuni za uchaguzi kuna sehemu ulikutana na neno mkwe wa rais

Golugwa: Hakuna

Ignas: Umeileza mahakama umewahi kukamatwa na hujawahi kufunguliwa hati ya mashitaka mahakamani

Golugwa: Ni kweli

Ignas: Ni kweli baada ya kusikilizwa polisi walikuachia

Golugwa baada ya mimi kutoa maelezo

Ignas: Na mara ya pili unasema ulikamatwa tarehe nane mwezi wa kumi na moja napo uliachiwa baada ya kusikilizwa maelezo yako

Golugwa: Ni kweli

Ignas: Umeleza elimu yoyote uliyonayo juu ya sheria

Golugwa: Sina elimu yoyote ya sheria

Ignas: Sasa umepata wapi ujasiri wa kuieleza mahakama mambo ya kisheria

Golugwa: Hata Layman anaweza kuongea na yuko mbele yako

Ignas: Ulieleza kuhusu ripoti za waangalizi ni za mwaka gani

Golugwa: zote ni za mwaka jana

Ignas: Wewe ni custodian wa hizo ripoti

Golugwa: Nilitafuta na kuzihifadhi

Ignas: Umezileta hapa mahakani

Golugwa: Hapana

Ignas: Hizo ripoti zipo kwa lugha gani

Golugwa: kwa kiingereza

Ignas: Utakubaliana na mimi wewe sio muandishi wa hizo ripoti

Golugwa: Ndio mimi sio muandishi wa hizo ripoti

Ignas: Hao walitoa ripoti kuna siku walikuita uzifasiri toka kingereza kwenda kiswahili

Golugwa: Kwanini na kwa sababu gani ni tafsiri

Ignas: Wewe hapa mahakamani umezielezea kwa kiswahili

Golugwa: Ndio

Ignas: Utakubaliana na mimi wewe form four ulipata grade gani kingereza

Golugwa: Sikumbuki

Ignas: Unatatizo la kumbukumbu

Golugwa: Ikihitajika ku refresh memory

Ignas: Je unafahamu mtu akifasiri inaweza kuharibu maana ya ripoti

Golugwa: Kama mtu akitafsiri vibaya yanaweza kuathiriwa au yasiathiriwe

Ignas: Umeelaza juu ya uwezo wako kwenye lugha ya kiingereza

Golugwa: Sio lazima

Ignas: Unafasiri document za kiingereza

Golugwa: Kingereza ulipata nini Golugwa C au D

Ignas: Sasa na D yako unataka kutafsiri ripoti kubwa kama hizi?

Golugwa: Ina shida gani

Ignas: Haya tuambie title ya ripoti ya Thabo mbeki kwa kiIngereza ilisemaje

Golugwa: Kwa kweli sikumbuki

Ignas: Tuje ile ripoti ya SADC wewe mfasiri inaitwaje

Golugwa: Kwa kingereza sikumbuki ila inazungumzia

Iganas: Kwa kingereza bwana wewe si mkalimani

Golugwa: Sikumbuki

Ignas: Uliweza kufuatiliwa ripoti ya waangalizi wa Jumuiya ya Afrika mashariki

Golugwa: Hapana

Ignas: Tukirudi kwenye hii ripoti ya Jaji Chande uliizungumzia jana swali langu ni kwamba una imani na ripoti hii

Golugwa: Sina imani nayo

Ignas: Kwa hiyo hata kile ulicho kieleza jana huna imani nacho licha kuwa kwenye ripoti ya Jaji Chande

Golugwa: Sikubaliana na wewe nilichokueleza mimi nina imani nacho licha kwamba sina imani na ripoti yote

Ignas: Inamaana kuna ambavyo vilikupendeza wewe

Golugwa: Hapana kitu gani hicho kuzungumzia

Ignas: Hebu turudi kwenye kikao cha watia nia uliongea habari ya unyunyu na makapi kulikuwa na habari ya manukato kwemye kikao chenu cha watia nia

Golugwa: Haikuwepo

Ignas: Waheshimiwa mimi nimemaliza watafuata wenzangu.

Leave a Comment