×

Rais Samia Apewa Pole na Viongozi Mbalimbali Baada Ya Kifo Cha Mumewe – Picha

Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) akimfariji Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026 kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

Viongozi, wageni mbalimbali, viongozi wa dini, wasanii na watu kutoka kada tofauti wamefika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia msiba wa mumewe, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Rais Samia amewasili nyumbani kwake Kizimkazi leo, Septemba 8, 2026, baada ya mumewe kufariki dunia Septemba 7, 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar.

Mtume Boniface Mwamposa pamoja na Mchungaji Tony Kapola wakimfariji Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

Miongoni mwa waliomtembelea Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye, ambaye alifika kutoa pole kufuatia msiba huo.

Viongozi wa dini pia wameungana na waombolezaji kumfariji Rais Samia, akiwemo Mtume Boniface Mwamposa pamoja na Mchungaji Tony Kapola.

Evariste Ndayishimiye, Rais wa Jamhuri ya Burundi akimfariji Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.
Wasanii mbalimbali wakimfariji Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Aidha, wasanii mbalimbali wamefika Kizimkazi kutoa pole na kumfariji Rais Samia katika kipindi hiki cha majonzi.

Msiba huo umeendelea kuwakutanisha viongozi na wageni mbalimbali wanaofika Kizimkazi kutoa pole kwa Rais Samia na familia ya Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Viongozi pamoja na Wageni mbalimbali wakimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.
Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Afrika CDC) Dkt. Jean Kaseya akimfariji  Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.
Viongozi pamoja na Wageni mbalimbali wakimfariji Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

 

Leave a Comment