Katuga: Unaimanini taarifa ya TLS
Heche: Ndio nina imamini
Katuga: Taarifa yetu inasema huyu bwana alitoweka tuambie uliona watu watu waliomteka
Heche: Mtuambie nyie watu wa serikali
Katuga: Nilikusikia umejitapa utasoma sheria
Heche: Ndio naanza
Katuga: Umewataja wengi sana ukiwaunganisha na mambo ya uchaguzi unakumbuka
Heche: Ndio
Katuga: Umewaambia majaji kwamba huyu kapotea sababu ya sheria za uchaguzi
Heche: Hapana
Katuga: Kila anayepotea anakuwa ametekwa
Heche: Niliozungumzia mimi ni waliotekwa
Katuga: Kila ambaye haonekani maetekwa
Heche: Sikuelewi
Katuga: Mke wa saimon anaitwa nani
Heche: Sikumbuki
Katuga: Iambie Mahakama kuwa ushahidi wa Bwana Simon kutekwa ni wa mke wake umeamiwa na mke wake
Heche: Sahihi
Katuga: Waambie majaji kama unajua ushahidi wa kuambiwa haukubaliki Mahakamani
Heche: Ndio
Katuga: Uanajua au hujui hata kusoma pia bado inakuwa hear say
Heche: Sijui
Katuga: Unajua hujui ushahdi wako lazima ulingane na facts
Heche: Najua
Katuga: Waambie majaji kama umetaja ya kesi ya mzee sasi.
Heche: Sikutaja
Katuga: Bwana mdogo nani alikupa zawadi ya jezi ya Arsenal yenye jina lako
Heche: Nmenunua mwenyewe
Katuga: Hiyo jezi umenunua wapi
Heche: Ya lini
Katuga: Na hiii
Heche: Nimekuambia tuko wengi baba yangu ana wake nane na tuko wengi
Katuga: Kuna mtu anaitwa Salman una mfahamu
Heche: Simfahamu
Katuga: Baada ya kupewa hela kwa ajili ya chama ulipeleka wapi
Heche: Sifahamu
Katuga: Ulisema mwaka 2024 Kamati Kuu ilikaa na kujadili bila mabadiliko hamtashiriki uchaguzi
Heche: Sahihi
Katuga: Mkurugenzi wa habari aliposema “No Reforms No Election” ilimaanisha kuzuia uchaguzi
Heche: Naweza kusema kinachonihusu
Jaji: Naomba usikilize kwa makini ujibu swali
Katuga:Wewe unaimbia Mahakama No Reforms No Election ni hakuna uchaguzi mpaka mabadiliko na Brenda alisema ilimaanisha kuzuia uchaguzi je kauli hizi ziko sawa au sio sawa.
Heche: Haziko sawa
Wakili Katuga: Waambie majaji, ile Prado ni ya shingapi?
Heche: Milioni 80.
Wakili Katuga: Na trekta?
Heche: Milioni 80.
Wakili Katuga: Ile Mitsubishi?
Heche: Milioni 60.
Wakili Katuga: Ulinunua ukiwa nani?
Heche: Makamu Mwenyekiti.
Wakili Katuga: Ni kweli kwamba kwa kipindi chote tangu umekuwa Makamu Mwenyekiti, hakuna fedha yoyote ambayo umelipwa?
Heche: Na nani?
Wakili Katuga: Waambie majaji, ni kweli ulieleza kwamba mdogo wako anaitwa Suguta?
Heche: Suguta.
Wakili Katuga: Wakati anakamatwa na polisi ulikuwepo?
Heche: Sikuwepo.
Wakili Katuga: Wakati ulisema alichomwa na singe ulikuwepo?
Heche: Alisema RPC.
Wakili Katuga: Ulikuwepo hukuwepo? Kwahiyo ni ushahidi wa RPC?
Heche: Sahihi.
Wakili Katuga: Waambie majaji kama huyu mdogo wako alichomwa na singe eneo gani la mwili?
Heche: Sikueleza.
Wakili Katuga: Umesema polisi walijaribu kumtupa mdogo wako ila walinzi walimuona?
Heche: Ni kweli.
Wakili Katuga: Waambie majaji kama ulikuwepo.
Heche: Sikuwepo.
Wakili Katuga: Huo ushahidi ulinetoa wapi?
Heche: RPC alieleza.
Wakili Katuga: Ni ushahidi wa RPC?
Heche: Wakwangu.
Wakili Katuga: Uliwahi kuhojiana na huyo polisi aliyemuua mdogo wako?
Heche: Ni sahihi.
Wakili Katuga: Alikueleza sababu za kufanya hilo tukio la kinyama? Kama alilenga kukuzuia wewe kwenye harakati za kisiasa.
Heche: Hakusema hivyo.
Wakili Katuga: Sababu za huyu bwana kutuhumiwa kufanya huo ukatili zimebaki kwa huyo mtuhumiwa, hapa Mahakamani hakuna?
Heche: Ni sahihi.
Wakili Katuga: Unajua au hujui, kwenye jinai, sababu za kumfanya mtu aachiliwe ni ushahidi?
Heche: Kuna rushwa, upendeleo, sababu ni nyingi.
Wakili Katuga: Umeiambia Mahakama hii tukufu kati ya hayo uliyosema ni sababu ipi ilipelekea huyu bwana polisi aachiliwe?
Heche: Ni upendeleo ndiyo uliyemwachia.
Wakili Katuga: Ulisema wewe unaamini kwamba waliomfanyia ukatili mdogo wako kwa kumuua, walikukomoa na kukuonyesha kwamba wanaweza kukufanyia chochote na wasifanywe chochote, huu ni ushahidi wa kuona, kusikia au imani?
Heche: (Hajajibu)
Wakili Katuga: Ana wazazi?
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Ni kweli kwamba uchungu wa mwana aijuaye mzazi?
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Kati ya wewe na mama yako aliyebeba ujauzito miezi tisa, nani anauchungu zaidi?
Heche: Hilo la mama kumuuliza yeye.
Wakili Katuga: Kwanini hukuiambia Mahakama kwamba huyu muuaji alitaka kumkomoa mama yako ila akataka kukukomoa wewe?
Heche: Alitaka kunikomoa.
Wakili Katuga: Kwahiyo wewe ndiye ulimsababishia kifo kwa sababu aliuliwa ili wewe utishike?
Heche: Alitaka niache siasa ndiyo maana akauliwa.
Wakili Katuga: Ulitokea mwaka gani?
Heche: 2018.
Wakili Katuga: Mwaka 2018 unakumbuka mambo ya siasa yalikuwa yamefungwa?
Heche: Nilikuwa mbunge, zilikuwa zinaendelea.
Wakili Katuga: Unakumbuka Magufuli alizuia siasa?
Heche: Alizuia mikutano ya hadhara, siyo siasa.
Wakili Katuga: Kwahiyo huyu polisi alimuua mdogo wako kukuzuia wewe kufanya siasa bungeni?
Heche: Popote.
Wakili Katuga: Wewe ni mjumbe wa Kamati Kuu?
Heche: Sahihi.
Wakili Katuga: Kikao cha tarehe 29/08/2026 ulihudhuria au hukuhudhuria?
Heche: Mpaka nilifresh.
Wakili Katuga: Kwahiyo unakumbuka vitu vya mwaka 2015 lakini vya 2026 haukumbuki? Heche: Baadhi nakumbuka baadhi sikumbuki, siyo vyote.
Wakili Katuga: Naibu Katibu Mkuu alisema tarehe 29/08/2026 kwamba kulikuwa na kikao cha Kamati Kuu na kilikusanya tonetone, ni kweli Kamati Kuu ilikaa?
Heche: Mwulize yeye, sikumbuki.
Wakili Katuga: Kuna kikao kilichokaa kikamueleza Golugwa aseme tonetone imefika milioni 302?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Unakumbuka au hukumbuki the same day unaletewa taarifa ya makusanyo ya tonetone na Naibu Katibu Mkuu alitoa maazimio, unakumbuka?
Heche: Wewe ni mjumbe wa Kamati Kuu? Si kweli.
Wakili Katuga: Kwahiyo taarifa ya Naibu Katibu Mkuu siyo taarifa ya Kamati Kuu?
Heche: Si kweli.
Wakili Katuga: Taarifa ya Naibu Katibu Mkuu ya kumtetea mwenyekiti wa chama kwa nguvu zote ni sahihi au siyo sahihi?
Heche: Siikumbuki hiyo taarifa.
Wakili Katuga: Uliwaambia majaji Ezekiel Wenje alinusurika kuuawa na akakimbilia Kenya?
Heche: Ni kweli.
Wakili Katuga: Wakati ananusurika ulikuwepo?
Heche: Sikuwepo.
Wakili Katuga: Ni aina gani sasa ya ushahidi huo?
Heche: Nilielezwa.
Wakili Katuga: Uliieleza mahakama ili ione huo ni ushahidi wa kweli?
Heche: Sikuieleza.
Wakili Katuga: Tunapomwita mtu mzalendo, ni yule ambaye anafanya kitu cha kizalendo kwenye nchi yake mama?
Heche: Sahihi.
Wakili Katuga: Mzalendo siyo mtu ambaye atahamasisha kuharibu nchi yake?
Heche: Upo sahihi.
Wakili Katuga: Mzalendo siyo mtu anayehamasisha uharibifu wa mali za umma?
Heche: Ni sahihi.
Wakili Katuga: Mzalendo wa kweli ni yule anayehamasisha shughuli za ujenzi wa taifa lake?
Heche: Wapo wanaofanya hivyo halafu siyo wazalendo.
Wakili Katuga: Mtu mzalendo ni yule anayehamasisha familia kufanya shughuli za maendeleo ya nchi yake?
Heche: Siyo lazima.
Wakili Katuga: Unajua au hujui Tanzania hatuna uraia pacha?
Heche: Naelewa.
Wakili Katuga: Unajua au hujui Mwenyekiti wako familia yake (watoto) siyo raia wa Tanzania?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Unajua mke wake si raia wa Tanzania?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Ulisema ulikamatwa nje ya Mahakama kwa tuhuma za kuvuka mpaka kwenda Kenya?
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Waambie majaji, je ni kweli ulivuka kwenda Kenya au hukuvuka?
Heche: Sikutaka.
Wakili Katuga: Ulitaka au hukutaka kwenda Kenya kupitia Sirali?
Heche: Nilitaka.
Wakili Katuga: Umeeleza hapa Mahakamani kwanini ulizuiliwa?
Heche: Sikueleza.
Wakili Katuga: Ulisema ulisafirishwa hadi Dodoma Kituo cha Polisi Mtumba selo ya peke yako, waambie majaji ulitaka uwekwe na nani? Na wewe ni mwanaume?
Heche: Ukisema kuwekwa na nani una maana gani?
Wakili Katuga: Katika kukamatwa kwako, uliwahi kuchukuliwa paspoti yako au hukuwahi?
Heche: Niliwahi.
Wakili Katuga: Lini ulichukuliwa?
Heche: Tarehe 18/10.
Wakili Katuga: Mwaka gani?
Heche: Mwaka jana.
Wakili Katuga: Ulirudishiwa?
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Ilikuwaje?
Heche: Niliandika barua kwa Kamishna Jenerali, wakanirudishia.
Wakili Katuga: Unajua au hujui DPP na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai wanasimamia jukumu la kuratibu upelelezi wa makosa ya jinai?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Kama hujui, ni kosa gani kisheria kuwakutanisha mawakili wa serikali na polisi?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Unajua au hujui, ulisema ulikutana nao Kituo cha Polisi Oysterbay?
Heche: Sahihi.
Wakili Katuga: Waambie majaji, unajua au hujui kwamba kesi ya jinai haina ukomo?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Pamoja na yote hakuwahi kushtakiwa, uliulizwa kushtakiwa kwenye matukio ya Oktoba 29 na matukio mengine ukajibu hakuwahi kushtakiwa, sasa unajua au hujui hawa mawakili walikuwa wanaratibu matukio ya Oktoba 29?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Unajua ama hujui watuhumiwa uliowaona pale walikuwa na makosa gani?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Unajua au hujui kama watuhumiwa wengine walikutana na wewe na viongozi wa CHADEMA kama waratibu wa matukio ya Oktoba 29?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Unajua au hujui, ushahidi uliokusanywa unaeleza ni wapi mlikaa vikao, wapi mipango ili kuratibu matukio ya Oktoba 29, 2025?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Ni ushahidi wako kwamba baada ya kuhojiwa kuhusiana na matendo ya kigaidi ulikataa?
Heche: Sikukataa.
Wakili Katuga: Maana ya nini?
Heche: Sikutoa maelezo.
Wakili Katuga: Ulikataa au hukakataa? Heche: Nilikataa.
Wakili Katuga: Ulisema ulisikia hotuba ya Jaji Chande, ulisikia kauli kwamba matukio yale yalipangwa na kuratibiwa?
Heche: Nilisikia.
Wakili Katuga: Unajua au hujui kwenye ushahidi uliokusanywa kama wewe ni mtuhumiwa wa uratibu wa matukio yale?
Heche: Mimi ni mshtakiwa au mtuhumiwa?
Wakili Katuga: Ulipatikana ushahidi kwamba wewe ulihusika kupanga na kuratibu matukio ya Oktoba 29, hotuba ya Chande ilisema yalipangwa na kuratibiwa sasa hivi vitu ni sawa au tofauti?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Nilikusikia ukisema hujui au huna kumbukumbu kama kuna viongozi wengine wa vyama vya siasa waliwahi kushtakiwa?
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Unamfahamu Zitto Kabwe?
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Ni wa chama gani?
Heche: ACT Wazalendo.
Wakili Katuga: Unajua au hujui kama Zitto Kabwe aliwahi kushtakiwa kwa kuchapisha taarifa za uongo?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Kwahiyo uliamua tu kusema?
Heche: Nilisema viongozi wa CCM.
Wakili Katuga: Basili Pesambili unamfahamu humfahamu?
Heche: Basili namfahamu.
Wakili Katuga: Unajua kama aliwahi kuwa waziri?
Heche: Sifahamu.
Wakili Katuga: Alafu unasema umewahi kuwa mbunge, tuambie kama unafahamu amewahi kushtakiwa?
Heche: Sifahamu hilo.
Wakili Katuga: Waambie majaji ile Hotel Dubai ulilala kwa shilingi ngapi?
Heche: Ipi? Dubai nimeenda mara nyingi.
Wakili Katuga: Waambie majaji, hapa nchini kwetu ili uende kutibiwa nje lazima uwe na referral ya hospitali zetu?
Heche: Kuna mtu anaamua tu kwenda nje.
Wakili Katuga: Waambie majaji kwa anayelipwa na serikali, ni lazima atimize wajibu au anaamua tu kwenda nje?
Heche: Lazima atimize yanayotakiwa.
Wakili Katuga: Kwahiyo mlipaji wa gharama za serikali, lazima ajiridhishe kwamba mtu huyo anakidhi vigezo vya referral ili aende nje? Kweli si kweli?
Heche: Nchi hii kuna upendeleo, siyo lazima.
Wakili Katuga: Unajua au hujui Mwenyekiti alipata referral kwenda nje au hujui?
Heche: Sijui.
Wakili Katuga: Ulisema Lissu alivuliwa ubunge.
Heche: Ndiyo.
Wakili Katuga: Unajua au hujui kama Lissu hakuridhika na maamuzi ya Spika, anaweza kwenda kupeleka shauri Mahakamani kwenda kupeleka pingamizi?
Heche: Najua.
Wakili Katuga: Unajua au hujui kama Lissu alipeleka shauri Mahakamani?
Heche: Sijui
Wakili Katuga: umesema no reforms no election ilitangazwa na Mbowe
Heche: Sahihi
Wakili Katuga: Waambie majaji kama, katika ushahidi wako,ulieleza au hukueleza kama mbowe alieleza kwamba tutazuia uchaguzi wa 2025
Heche: Sikueleza
Wakili Katuga: Kama alisema watahamasisha uasi
Heche: Hakusema
Wakili Katuga: Waambie majaji kama mbowe alielezea suala la kukinukisha?
Heche: Hakusema
Wakili Katuga: Waambie majaji kama kwenye huo msimamo kuna maneno kwamba tutazuia uchaguzi
Heche: Hakuna
Wakili Katuga: Waambie kama kwenye maneno no reforms no kuna maneno kwamba tunaenda kuhamasisha uasi
Heche: Hapana
Wakili Katuga: Je, tunaenda kukinukisha vibaya sana?
Heche: Inategemeana na context yako na mtu anavyoelewa
