×

Katuga Ambana Heche Maswali ya Mauaji ya Mawazo na Akwilina

Katika kuendelea kutoa ushahidi katika kesi inayomkabili Tundu Lissu, shahidi John Heche amekabiliwa na maswali makali kutoka kwa Wakili Katuga kuhusu kauli mbalimbali alizowahi kutoa kuhusu mauaji ya Alphonce Mawazo, Akwilina Akwilina na Msafiri Mbwambo, pamoja na matukio mengine ya kisiasa nchini.

Katika mahojiano hayo, Katuga alimuuliza Heche iwapo ana imani na Mahakama, ambapo Heche alisema anaamini Mahakama, huku akieleza kuwa hawezi kusema kwa kiwango gani ana imani nayo kwa kuwa kesi bado haijaamuliwa.

Wakili Katuga pia alimuuliza Heche kuhusu kauli alizowahi kutoa hadharani kuhusu kesi hiyo, akimtaka kukumbuka baadhi ya hotuba na video zilizopo mtandaoni. Heche alipoonyeshwa baadhi ya video, alihoji matumizi ya teknolojia ya AI, huku akisema baadhi ya sauti alizozisikia zilifanana na yake.

Katika sehemu nyingine ya mahojiano, Katuga alimuuliza Heche kuhusu kifo cha Msafiri Mbwambo, ambaye shahidi alidai aliuawa kwa sababu za kisiasa na zinazohusiana na uchaguzi. Heche alieleza kuwa taarifa hizo alizipata kupitia mijadala mbalimbali, ikiwemo Bungeni na vyombo vya habari.

Heche pia aliulizwa kuhusu mauaji ya Alphonce Mawazo, ambapo alisema alifahamu kuwa kifo chake kilihusishwa na uchaguzi kwa sababu Mawazo alikuwa kwenye kampeni. Hata hivyo, alipoulizwa chanzo cha taarifa hizo, Heche alisema suala hilo lilijadiliwa katika maeneo mbalimbali na kuandikwa na vyombo vya habari.

Kuhusu mauaji ya Akwilina Akwilina mwaka 2018, Katuga alimuuliza Heche kuhusu tukio hilo lililotokea wakati wa kampeni za uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni. Heche alithibitisha kuwa siku hiyo CHADEMA ilikuwa ikihitimisha kampeni.

Katuga pia alimuuliza iwapo baada ya mkutano kulikuwa na kundi la watu lililoelekea Magomeni na kutawanywa na polisi. Heche alikiri kuwa kulikuwa na kundi hilo na kwamba polisi waliwataka watawanyike.

Katika hatua nyingine, Katuga alimuuliza Heche kuhusu madai ya kuwepo kwa kesi dhidi ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA zinazohusiana na madai ya kutekwa kwa watu, akiwemo Bariki na Paul Mafie. Heche alisema hafahamu kuhusu suala hilo.

Mahojiano hayo yamejikita zaidi katika chanzo na msingi wa taarifa ambazo Heche amezitoa mahakamani, huku upande wa mashtaka ukitaka kubaini kama baadhi ya madai yake yanatokana na ushahidi aliouona mwenyewe au taarifa alizosoma na kusikia kutoka kwa vyanzo vingine.

Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa mahakamani.

Katuga: Unajua ama hujui Tanzania ni nchi huru

Heche: Najua

Katuga Unajua hujui kwa mujibu wa Katiba ya 77 Mahakama ndio chombo kinachotoa haki

Heche: Najua

Katuga: Unajua Mahakama haitakiwi kuingiliwa

Heche: Najua

Katuga: Unaimani na hii Mahakama

Heche: Kesi haijaamulIwa siwezi sema nina imani

Katuga: Waambie Majaji unaiaminini huiamini

Heche: Naimini

Katuga: Je ni sahihi kisheria mtu anayekuja kuwa shahidi akamapima dimina ya majaji

Heche: Sijui

Katuga: Waambie majaji kama uko hapa baada ya Lissu kuonekakana na kesi ya kujibu

Heche: Najua

Katuga: Unajua kwamba ushahidi wa kielectromic ni sawa na document

Heche: Sifahamu

Katuga: Waambie majaji kama hotuba zako nyingi ziko mtandaoni

Heche: Najua

Katuga: Waambie majaji kama uliwahi kuongelea kesi hii baada ya mshitakiwa kupatikana na kesi ya kujibu

Heche: Sikumbuki

Katuga: Waambie majaji kama ulisema dimina ya jaji haiko sawa hata ukimuangalia

Heche: Sikumbuki

Katuga: Uko tayari tukusikilizishe

Heche: Sikuamini kuna AI siku hizi

Katuga: Waheshimiwa Majaji naomba tumuoneshe fresh memory ili atusaidie kujibu baada ya maswali

Jaji: Endelea

Lissu: Huu utaratibu sijaelewa uko kwa sheria gani

Jaji: Utamfanyia re-examination

Heche: Siwezi kuamini kompyuta ni Katuga zama hizi za AI waheshimiwa majaji

Jaji: Wewe sikiliza kisha utafafanua

Katuga: Hii hotuba unaikumbuka

Heche: Kwa mbaali sauti kama ni yangu

Katuga: Unaikumbuka huiumbuki

Heche: Siiikumbuki

Katuga: Unakumbuka ulisema shahidi wa 17 yeye ndio amepublish

Heche: Ndio

Katuga: Je hilo swala shahidi ya 17 limezungumziwa hapo kwenye video

Heche: Hiyo video sio yangu

Katuga: Walau jibu kidogo hayo maneno P17 alisema ndiye alipublish yanafanana ya ushahdi wako hayafanani

Heche: Nimeyasikia yanafanana kwenye hiyo AI yako

Katuga: Kuthibitisha na ku-establish premafasheee kesi nini maana yake

Heche: Sijui maana yake

Katuga: Waambie majaji kama uliridhika Mahakama Ilipoamua Lissu anakesi ya kujibu uliridhika au hukuridhika

Heche: Sikuridhika

Katuga: Uliwahi kuita press kuwasema mashahidi waongo hapo nje

Heche: Hapana

Katuga: Tukikuonesha tena utakubali au utaita AI

Heche: Siwezi kukataa kama ni kitu cha kweli

Katuga: Lissu anachombo cha habari

Heche: Hapana

Katuga: Lissu akitaka kupeleka ujumbe kwa uma anatumia njia gani

Heche: Anatumia mikutano

Katuga: Mh Lissu akitaka kupeleka ujumbe kwa watanzania wote anatumia vyombo vya habari

Heche: Anahutubia mikutano

Katuga: Kwenye ushahdi wako ulisema mapolisi walikuwa wanaingiza kura feki kwenye vibegi vyao embu waambie majaji kama uliwahi kumkamata

Heche: Niliwahi kuona askari shule ya Msingi Nyanungu

Katuga: Ulileta huo ushahidi hapa mahakamani

Heche: Niliongea general

Katuga: Na unataka Mahakama ikuamini

Heche: Ndio

Katuga: Unajua watu wanatuhuma za mauaji kwa sababu mbali mbali

Heche: Najua

Katuga: Katika ushahiri wako umeiambia Mahakama hii Msafiri Mbwambo alichinjwa kwa kulalamikia sheria za uchaguzi

Heche: Aliuawa sababu ya siasa

Katuga: Uliwaambia majaji ameuawa sababu ya moja mbili tatu

Heche: Nilisema sababu ya sababu za kisiasa

Katuga: Umeeleza ile sababu ya msingi, waambie majaji kama umeelezea sababu yake ya kuchinjwa

Heche: Nilieleza sababu za kiuchaguzi

Katuga: Unajua au hujui kuna kesi kwa viongozi wa CHADEMA iko Arusha ya kuteka mtu anaitwa Bariki na Paul Mafie na kuwapandisha mlimani kwa nia ya kuwatesa na kuwatishia unajua au hujui

Heche: Sifahamu

Katuga: Unajua mtu yoyote anaweza kushitakiwa kwa jinai

Heche: Najua

Katuga: Unajua kusadikika ni hisia

Heche: Ndio

Katuga: Ushahadi wako Katibu wenu aliuawa na watu wanaosadikika ni wa CCM

Heche: Nilisema sababu za kiuchaguzi

Katuga: Nani anafuatilia viapo vya mawakala Chadema

Heche: Kila eneo linafuatiliaji wake, mgombea, kiongozi wa chama kulingana na eneo husika

Katuga: Mwaka 2018 wakati wa kampeni za Jimbo la Kinondoni, alikuwa mgombea ni nani

Heche: Salum Mwalimu

Katuga: Ni kweli kwamba siku Akwilina ameuawa mlikuwa mnafunga kampeni

Heche: Ni kweli

Katuga: Waambie majaji kama sio kweli jioni baada ya mkutano ilitoka hamasa ya kwenda kwa Mkurugenzi kwa maandamano

Heche: Sio kweli

Katuga: Waambie majaji kama uliwaambia majaji mlikuwa watu wa ngapi mkifuata kwenda Magomeni

Heche: Hapana

Katuga: Ni kweli kwamba mlikuwa Kundi, ikabidi polisi wa wawatawanye

Heche: Ndio ni kweli

Katuga: Wakati mnashitakiwa 2018 ulisema Mwenyekiti alikuwa ameshambuliwa

Heche: Nilisema Mwenyekiti wetu wa sasa

Katuga: Ulisema angekuwa ameshambuliwa kwa risasi tungekuwa naye huu ni ushahidi wa aina gani ni ku- assune, kuona au kusikikiii

Heche: Kuamini

Katuga: Ulijua muaji wa Alphonce Mawazo

Heche: Hapana

Katuga: Waambie Mahakama kama ulijua sababu

Heche: Ilikuwa uchaguzi

Katuga: Sasa ulijuaje hizo sababu

Heche: Sababu ya uchaguzi alikuwa kwenye kampeni

Katuga: Mtu mwenye ugomvi na Mawazo anaruhusiwa kuua wakati wa uchaguzi

Heche: Sheria inakuzuia wakati wote

Katuga: Kwa hiyo huu ushahidi wa Mawazo ni wako au wa kusoma

Heche: NIlisoma na iljadiliwa Bungeni

Katuga: Unaawaambia Majaji ushahidi wako ni sababu za Bungeni

Heche: Ni ushahidi wangu ni sababu za uchaguzi

Katuga: Waambie majaji hizo sababu za hayo mauaji umetoa wapi

Heche: Ilijadiliwa kila mahali na hata kuandikwa kwenye vyombo vya habari

Katuga: Unaimanini taarifa ya TLS

Heche: Ndio nina imamini

Katuga: Taarifa yetu inasema huyu bwana alitoweka tuambie uliona watu watu waliomteka

Heche: Mtuambie nyie watu wa serikali

Katuga: Nilikusikia umejitapa utasoma sheria

Heche: Ndio naanza

Katuga: Umewataja wengi sana ukiwaunganisha na mambo ya uchaguzi unakumbuka

Heche: Ndio

Katuga: Umewaambia majaji kwamba huyu kapotea sababu ya sheria za uchaguzi

Heche: Hapana

Katuga: Kila anayepotea anakuwa ametekwa

Heche: Niliozungumzia mimi ni waliotekwa

Katuga: Kila ambaye haonekani maetekwa

Heche: Sikuelewi

Katuga: Mke wa saimon anaitwa nani

Heche: Sikumbuki

Katuga: Iambie Mahakama kuwa ushahidi wa Bwana Simon kutekwa ni wa mke wake umeamiwa na mke wake

Heche: Sahihi

Katuga: Waambie majaji kama unajua ushahidi wa kuambiwa haukubaliki Mahakamani

Heche: Ndio

Katuga: Uanajua au hujui hata kusoma pia bado inakuwa hear say

Heche: Sijui

Katuga: Unajua hujui ushahdi wako lazima ulingane na facts

Heche: Najua

Katuga: Waambie majaji kama umetaja ya kesi ya mzee sasi.

Heche: Sikutaja

Katuga: Bwana mdogo nani alikupa zawadi ya jezi ya Arsenal yenye jina lako

Heche: Nmenunua mwenyewe

Katuga: Hiyo jezi umenunua wapi

Heche: Ya lini

Katuga: Na hiii

Heche: Nimekuambia tuko wengi baba yangu ana wake nane na tuko wengi

Katuga: Kuna mtu anaitwa Salman una mfahamu

Heche: Simfahamu

Katuga: Baada ya kupewa hela kwa ajili ya chama ulipeleka wapi

Heche: Sifahamu

Katuga: Ulisema mwaka 2024 Kamati Kuu ilikaa na kujadili bila mabadiliko hamtashiriki uchaguzi

Heche: Sahihi

Katuga: Mkurugenzi wa habari aliposema “No Reforms No Election” ilimaanisha kuzuia uchaguzi

Heche: Naweza kusema kinachonihusu

Jaji: Naomba usikilize kwa makini ujibu swali

Katuga:Wewe unaimbia Mahakama No Reforms No Election ni hakuna uchaguzi mpaka mabadiliko na Brenda alisema ilimaanisha kuzuia uchaguzi je kauli hizi ziko sawa au sio sawa.

Heche: Haziko sawa

Wakili Katuga: Waambie majaji, ile Prado ni ya shingapi?

Heche: Milioni 80.

Wakili Katuga: Na trekta?

Heche: Milioni 80.

Wakili Katuga: Ile Mitsubishi?

Heche: Milioni 60.

Wakili Katuga: Ulinunua ukiwa nani?

Heche: Makamu Mwenyekiti.

Wakili Katuga: Ni kweli kwamba kwa kipindi chote tangu umekuwa Makamu Mwenyekiti, hakuna fedha yoyote ambayo umelipwa?

Heche: Na nani?

Wakili Katuga: Waambie majaji, ni kweli ulieleza kwamba mdogo wako anaitwa Suguta?

Heche: Suguta.

Wakili Katuga: Wakati anakamatwa na polisi ulikuwepo?

Heche: Sikuwepo.

Wakili Katuga: Wakati ulisema alichomwa na singe ulikuwepo?

Heche: Alisema RPC.

Wakili Katuga: Ulikuwepo hukuwepo? Kwahiyo ni ushahidi wa RPC?

Heche: Sahihi.

Wakili Katuga: Waambie majaji kama huyu mdogo wako alichomwa na singe eneo gani la mwili?

Heche: Sikueleza.

Wakili Katuga: Umesema polisi walijaribu kumtupa mdogo wako ila walinzi walimuona?

Heche: Ni kweli.

Wakili Katuga: Waambie majaji kama ulikuwepo.

Heche: Sikuwepo.

Wakili Katuga: Huo ushahidi ulinetoa wapi?

Heche: RPC alieleza.

Wakili Katuga: Ni ushahidi wa RPC?

Heche: Wakwangu.

Wakili Katuga: Uliwahi kuhojiana na huyo polisi aliyemuua mdogo wako?

Heche: Ni sahihi.

Wakili Katuga: Alikueleza sababu za kufanya hilo tukio la kinyama? Kama alilenga kukuzuia wewe kwenye harakati za kisiasa.

Heche: Hakusema hivyo.

Wakili Katuga: Sababu za huyu bwana kutuhumiwa kufanya huo ukatili zimebaki kwa huyo mtuhumiwa, hapa Mahakamani hakuna?

Heche: Ni sahihi.

Wakili Katuga: Unajua au hujui, kwenye jinai, sababu za kumfanya mtu aachiliwe ni ushahidi?

Heche: Kuna rushwa, upendeleo, sababu ni nyingi.

Wakili Katuga: Umeiambia Mahakama hii tukufu kati ya hayo uliyosema ni sababu ipi ilipelekea huyu bwana polisi aachiliwe?

Heche: Ni upendeleo ndiyo uliyemwachia.

Wakili Katuga: Ulisema wewe unaamini kwamba waliomfanyia ukatili mdogo wako kwa kumuua, walikukomoa na kukuonyesha kwamba wanaweza kukufanyia chochote na wasifanywe chochote, huu ni ushahidi wa kuona, kusikia au imani?

Heche: (Hajajibu)

Wakili Katuga: Ana wazazi?

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Ni kweli kwamba uchungu wa mwana aijuaye mzazi?

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Kati ya wewe na mama yako aliyebeba ujauzito miezi tisa, nani anauchungu zaidi?

Heche: Hilo la mama kumuuliza yeye.

Wakili Katuga: Kwanini hukuiambia Mahakama kwamba huyu muuaji alitaka kumkomoa mama yako ila akataka kukukomoa wewe?

Heche: Alitaka kunikomoa.

Wakili Katuga: Kwahiyo wewe ndiye ulimsababishia kifo kwa sababu aliuliwa ili wewe utishike?

Heche: Alitaka niache siasa ndiyo maana akauliwa.

Wakili Katuga: Ulitokea mwaka gani?

Heche: 2018.

Wakili Katuga: Mwaka 2018 unakumbuka mambo ya siasa yalikuwa yamefungwa?

Heche: Nilikuwa mbunge, zilikuwa zinaendelea.

Wakili Katuga: Unakumbuka Magufuli alizuia siasa?

Heche: Alizuia mikutano ya hadhara, siyo siasa.

Wakili Katuga: Kwahiyo huyu polisi alimuua mdogo wako kukuzuia wewe kufanya siasa bungeni?

Heche: Popote.

Wakili Katuga: Wewe ni mjumbe wa Kamati Kuu?

Heche: Sahihi.

Wakili Katuga: Kikao cha tarehe 29/08/2026 ulihudhuria au hukuhudhuria?

Heche: Mpaka nilifresh.

Wakili Katuga: Kwahiyo unakumbuka vitu vya mwaka 2015 lakini vya 2026 haukumbuki? Heche: Baadhi nakumbuka baadhi sikumbuki, siyo vyote.

Wakili Katuga: Naibu Katibu Mkuu alisema tarehe 29/08/2026 kwamba kulikuwa na kikao cha Kamati Kuu na kilikusanya tonetone, ni kweli Kamati Kuu ilikaa?

Heche: Mwulize yeye, sikumbuki.

Wakili Katuga: Kuna kikao kilichokaa kikamueleza Golugwa aseme tonetone imefika milioni 302?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Unakumbuka au hukumbuki the same day unaletewa taarifa ya makusanyo ya tonetone na Naibu Katibu Mkuu alitoa maazimio, unakumbuka?

Heche: Wewe ni mjumbe wa Kamati Kuu? Si kweli.

Wakili Katuga: Kwahiyo taarifa ya Naibu Katibu Mkuu siyo taarifa ya Kamati Kuu?

Heche: Si kweli.

Wakili Katuga: Taarifa ya Naibu Katibu Mkuu ya kumtetea mwenyekiti wa chama kwa nguvu zote ni sahihi au siyo sahihi?

Heche: Siikumbuki hiyo taarifa.

Wakili Katuga: Uliwaambia majaji Ezekiel Wenje alinusurika kuuawa na akakimbilia Kenya?

Heche: Ni kweli.

Wakili Katuga: Wakati ananusurika ulikuwepo?

Heche: Sikuwepo.

Wakili Katuga: Ni aina gani sasa ya ushahidi huo?

Heche: Nilielezwa.

Wakili Katuga: Uliieleza mahakama ili ione huo ni ushahidi wa kweli?

Heche: Sikuieleza.

Wakili Katuga: Tunapomwita mtu mzalendo, ni yule ambaye anafanya kitu cha kizalendo kwenye nchi yake mama?

Heche: Sahihi.

Wakili Katuga: Mzalendo siyo mtu ambaye atahamasisha kuharibu nchi yake?

Heche: Upo sahihi.

Wakili Katuga: Mzalendo siyo mtu anayehamasisha uharibifu wa mali za umma?

Heche: Ni sahihi.

Wakili Katuga: Mzalendo wa kweli ni yule anayehamasisha shughuli za ujenzi wa taifa lake?

Heche: Wapo wanaofanya hivyo halafu siyo wazalendo.

Wakili Katuga: Mtu mzalendo ni yule anayehamasisha familia kufanya shughuli za maendeleo ya nchi yake?

Heche: Siyo lazima.

Wakili Katuga: Unajua au hujui Tanzania hatuna uraia pacha?

Heche: Naelewa.

Wakili Katuga: Unajua au hujui Mwenyekiti wako familia yake (watoto) siyo raia wa Tanzania?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Unajua mke wake si raia wa Tanzania?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Ulisema ulikamatwa nje ya Mahakama kwa tuhuma za kuvuka mpaka kwenda Kenya?

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Waambie majaji, je ni kweli ulivuka kwenda Kenya au hukuvuka?

Heche: Sikutaka.

Wakili Katuga: Ulitaka au hukutaka kwenda Kenya kupitia Sirali?

Heche: Nilitaka.

Wakili Katuga: Umeeleza hapa Mahakamani kwanini ulizuiliwa?

Heche: Sikueleza.

Wakili Katuga: Ulisema ulisafirishwa hadi Dodoma Kituo cha Polisi Mtumba selo ya peke yako, waambie majaji ulitaka uwekwe na nani? Na wewe ni mwanaume?

Heche: Ukisema kuwekwa na nani una maana gani?

Wakili Katuga: Katika kukamatwa kwako, uliwahi kuchukuliwa paspoti yako au hukuwahi?

Heche: Niliwahi.

Wakili Katuga: Lini ulichukuliwa?

Heche: Tarehe 18/10.

Wakili Katuga: Mwaka gani?

Heche: Mwaka jana.

Wakili Katuga: Ulirudishiwa?

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Ilikuwaje?

Heche: Niliandika barua kwa Kamishna Jenerali, wakanirudishia.

Wakili Katuga: Unajua au hujui DPP na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai wanasimamia jukumu la kuratibu upelelezi wa makosa ya jinai?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Kama hujui, ni kosa gani kisheria kuwakutanisha mawakili wa serikali na polisi?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Unajua au hujui, ulisema ulikutana nao Kituo cha Polisi Oysterbay?

Heche: Sahihi.

Wakili Katuga: Waambie majaji, unajua au hujui kwamba kesi ya jinai haina ukomo?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Pamoja na yote hakuwahi kushtakiwa, uliulizwa kushtakiwa kwenye matukio ya Oktoba 29 na matukio mengine ukajibu hakuwahi kushtakiwa, sasa unajua au hujui hawa mawakili walikuwa wanaratibu matukio ya Oktoba 29?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Unajua ama hujui watuhumiwa uliowaona pale walikuwa na makosa gani?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Unajua au hujui kama watuhumiwa wengine walikutana na wewe na viongozi wa CHADEMA kama waratibu wa matukio ya Oktoba 29?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Unajua au hujui, ushahidi uliokusanywa unaeleza ni wapi mlikaa vikao, wapi mipango ili kuratibu matukio ya Oktoba 29, 2025?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Ni ushahidi wako kwamba baada ya kuhojiwa kuhusiana na matendo ya kigaidi ulikataa?

Heche: Sikukataa.

Wakili Katuga: Maana ya nini?

Heche: Sikutoa maelezo.

Wakili Katuga: Ulikataa au hukakataa? Heche: Nilikataa.

Wakili Katuga: Ulisema ulisikia hotuba ya Jaji Chande, ulisikia kauli kwamba matukio yale yalipangwa na kuratibiwa?

Heche: Nilisikia.

Wakili Katuga: Unajua au hujui kwenye ushahidi uliokusanywa kama wewe ni mtuhumiwa wa uratibu wa matukio yale?

Heche: Mimi ni mshtakiwa au mtuhumiwa?

Wakili Katuga: Ulipatikana ushahidi kwamba wewe ulihusika kupanga na kuratibu matukio ya Oktoba 29, hotuba ya Chande ilisema yalipangwa na kuratibiwa sasa hivi vitu ni sawa au tofauti?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Nilikusikia ukisema hujui au huna kumbukumbu kama kuna viongozi wengine wa vyama vya siasa waliwahi kushtakiwa?

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Unamfahamu Zitto Kabwe?

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Ni wa chama gani?

Heche: ACT Wazalendo.

Wakili Katuga: Unajua au hujui kama Zitto Kabwe aliwahi kushtakiwa kwa kuchapisha taarifa za uongo?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Kwahiyo uliamua tu kusema?

Heche: Nilisema viongozi wa CCM.

Wakili Katuga: Basili Pesambili unamfahamu humfahamu?

Heche: Basili namfahamu.

Wakili Katuga: Unajua kama aliwahi kuwa waziri?

Heche: Sifahamu.

Wakili Katuga: Alafu unasema umewahi kuwa mbunge, tuambie kama unafahamu amewahi kushtakiwa?

Heche: Sifahamu hilo.

Wakili Katuga: Waambie majaji ile Hotel Dubai ulilala kwa shilingi ngapi?

Heche: Ipi? Dubai nimeenda mara nyingi.

Wakili Katuga: Waambie majaji, hapa nchini kwetu ili uende kutibiwa nje lazima uwe na referral ya hospitali zetu?

Heche: Kuna mtu anaamua tu kwenda nje.

Wakili Katuga: Waambie majaji kwa anayelipwa na serikali, ni lazima atimize wajibu au anaamua tu kwenda nje?

Heche: Lazima atimize yanayotakiwa.

Wakili Katuga: Kwahiyo mlipaji wa gharama za serikali, lazima ajiridhishe kwamba mtu huyo anakidhi vigezo vya referral ili aende nje? Kweli si kweli?

Heche: Nchi hii kuna upendeleo, siyo lazima.

Wakili Katuga: Unajua au hujui Mwenyekiti alipata referral kwenda nje au hujui?

Heche: Sijui.

Wakili Katuga: Ulisema Lissu alivuliwa ubunge.

Heche: Ndiyo.

Wakili Katuga: Unajua au hujui kama Lissu hakuridhika na maamuzi ya Spika, anaweza kwenda kupeleka shauri Mahakamani kwenda kupeleka pingamizi?

Heche: Najua.

Wakili Katuga: Unajua au hujui kama Lissu alipeleka shauri Mahakamani?

Heche: Sijui

Wakili Katuga: umesema no reforms no election ilitangazwa na Mbowe

Heche: Sahihi

Wakili Katuga: Waambie majaji kama, katika ushahidi wako,ulieleza au hukueleza kama mbowe alieleza kwamba tutazuia uchaguzi wa 2025

Heche: Sikueleza

Wakili Katuga: Kama alisema watahamasisha uasi

Heche: Hakusema

Wakili Katuga: Waambie majaji kama mbowe alielezea suala la kukinukisha?

Heche: Hakusema

Wakili Katuga: Waambie majaji kama kwenye huo msimamo kuna maneno kwamba tutazuia uchaguzi

Heche: Hakuna

Wakili Katuga: Waambie kama kwenye maneno no reforms no kuna maneno kwamba tunaenda kuhamasisha uasi

Heche: Hapana

Wakili Katuga: Je, tunaenda kukinukisha vibaya sana?

Heche: Inategemeana na context yako na mtu anavyoelewa

Leave a Comment