×

Mtoto wa Zidane aanza yake Real Madrid

1392947_originalMADRID, Hispania

MTOTO wa Kocha wa Real Madr id, Zinedine Zidane, anayejulikana kwa jina la Enzo, juzi al­iichezea timu hiyo mchezo wake wa kwanza na kufani­kiwa kupachika bao muhimu kwa timu hiyo.

Real ilivaana na Cultural Leonesa kwenye mchezo wa Kombe la Copa del Rey, ambapo Enzo alifanikiwa kufun­ga bao hilo dakika 18 tu tangu aingie uwanjani.

Enzo ambaye kwa sasa na umri wa miaka 21, anaamini kuwa anaweza kuja kuwa mchezaji ma­hiri siku za usoni na alifunga bao hilo katika shuti lake la kwanza kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu.

Madrid walifani­kiwa kupata ushindi wa mabao 6-1, iki­wa wamewachapa wapinzani hao wa­naoshiriki Ligi Dara­ja la Pili kwa jumla ya mabao 13-2, baa­da ya kushinda 7-1 kwenye mchezo wa kwanza.

Enzo ambaye ni mtoto mkubwa wa Zidane amefanikiwa kuichezea timu ya akiba ya Real mich­ezo 50, huu ndiyo ulikuwa mchezo wake wa kwanza kuichezea timu ya wakubwa.

halotel-strip-1-1