DAR ES SALAA: TIMU ya Simba SC yenye makao yake makuu Mtaa wa Msimbazi, imerejea leo jijini Dar es Salaam ikitokea Visiwani Zanzibar baada ya kumalizika kwa mashindano ya Kombe la Mapinduzi.
Simba imerejea nyumbani ikiwa imenyong’onyea kufuatia kipigo ilichokipata jana kutoka kwa wanaramabaramba, Azam FC ambao iliiyoinyuka Simba kwa bao 1-0, bao pekee lililofungwa na dakika ya 13 na kiungo Himid Mao ‘Ninja’ ambalo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo na kuwafanya Azam kutwaa ubinwa wa michuano hiyo.
Hapa nimekuwekea picha za Simba walivyowasili leo kwenye Bandari ya Dar es Salaam kwa usafiri wa Boti ya MV Azam.
Comments are closed.