×

Wanafunzi Watinga Global Kujifunza Taaluma Ya Habari

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Marian Girls iliyoko Bagamoyo Mkoani Pwani wakiwa katika ofisi za Global wakiendelea kupata maelezo kutoka kwa Mhariri wa Ijumaa Wikienda, Sifael Paul (katikati).

KWA siku mbili mfulululizo, baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Marian Girls iliyoko Bagamoyo Mkoani Pwani, wamefika katika  Ofisi za Magazeti ya Global Publishers kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali juu namna kazi za kukusanya na kuandika habari zinafanyika, ikiwa ni pamoja na mchango wa tasnia hiyo kwenye jamii.

Wanafunzi hao wakiendelea kuselfika na Mhariri Mtendaji wa Global, Saleh Ally.

Katika kufanikisha hilo, wanafunzi hao walipata fursa ya kuhudhuria moja ya vikao vya uboreshaji wa magazeti hayo, ambayo ni Uwazi, Ijumaa, Amani, Risasi, Ijumaa Wikienda, Risasi Jumamosi, Championi Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumamosi ikiwa ni sehemu ya kukamilisha mafunzo yao.

Siku ya pili, wakiwa na shauku ya kujua mambo mengi, walikutana na mmoja wa wahariri waandamizi, Siafel Paul na kumuuliza mambo mbalimbali na kujibiwa sawia, jambo ambalo walishukuru kwa mapokezi na ushirikiano ambao wamepewa.

Wakiwa katika picha ya pamoja.

“Hakika tumejifunza mambo mengi, mengine ni tofauti kabisa na ambayo tulitaka kujua, tunashukuru kwa mapokezi na ushirikiano huu ambapo kwa kweli tumejifunza elimu kubwa mno,” walisema wanafunzi hao wakionesha moyo na siha za furaha.

(Habari: Brighton Masalu/GPL)

 

Leave a Comment