
CCM tunaridhiswa sana na utendaji wa Serikali ya Rais @MagufuliJP kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa kati, uwepo wa viwanda –@hpolepole pic.twitter.com/JWYAfUBP9q
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 29, 2017
Katika hatua nyingine, Polepole amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaunga Mkono Kauli ya Rais Magufuli ya kutorudi masomoni kwa wanafunzi waliopata ujauzito wakiwa shule kwenye mfumo rasmi wa Elimu.
Polepole amesema kuwa wanafunzi waliopata ujauzito hawataweza kurudi shuleni kwenye mfumo rasmi isipokuwa kwenye Mfumo wa elimu ya watu wazima.
Tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, viwanda zaidi ya 370 vimejegwa, 89 vikubwa, vingi vimejengwa na sekta binafsi-@hpolepole pic.twitter.com/XT6caLSImh
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 29, 2017