
MHAMASISHAJI mashuhuri wa kimataifa na Mwenyekiti Mtendaji wa Mawasiliano ya Simu ya Econet na Vyombo vya Habari na Teknolojia Dk. Strive Masiyiwa, jana usiku alielezea mbinu mbalimbali zinazoweza kuwafanya vijana kuondokana na umaskini.

Aliyasema hayo katika semina iliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, ambapo jumla ya washiriki 500 walihudhuria kujifunza mambo mbalimbali ya kiuchumi na kimaendeleo, wengi wao wakiwa vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali nchini.

Aidha, Dk. Masiyiwa alifafanua namna vijana wanavyoweza kutoka hatua moja hadi nyingine ya kimaendeleo kupitia fursa wanazozifanya, na alielezea kirefu elimu ya ushauri wa kimawazo katika jamii ambayo ni muhimu kwa kuwajenga wajasiriamali barani Afrika.



NA DENIS MTIMA | GLOBAL PUBLISHERS