×

VIDEO: Rais Magufuli Awataka Wakimbizi wa Burundi Warudi Kwao

Rais John Magufuli na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza.

 

Rais John Magufuli amemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba kusimamisha kuwapa uraia raia wa Burundi kuanzia sasa na kuwaomba warejee kwao kama alivyowataka Rais wa Burundi Pierre Nkurunzinza kwa vile nchini humo sasa amani imerejea.


Hayo ameyasema leo, Alhamisi Julai 20 wakati akizungumza katika Uwanja wa Mpira wa Lemela, Ngara alipokwenda kwa ziara yake mkoani Kagera, akiwa ameambatana na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza.

“Rais amezungumza hapa kwa upole, Rais mwenyewe ana hofu ya Mungu, wazazi wake waliuawa, lakini anataka kushirikiana na Warundi wote kwa nini mnataka kuondoka kwenu?

“Naomba Warundi mrudi nyumbani, mkashirikiane na wenzenu kuijenga Burundi. Nchi ina amani sasa, wala asitokee mtu akawadanganya kwamba kuna machafuko. Hatuwafukuzi lakini tunawaomba muende kwa amani, nyinyi ni ndugu zetu,” alisema Magufuli.


Awali, Rais Nkurunziza amezungumza na wananchi hao na kuwataka raia wa Burundi warudi nchini mwao kwani kwa sasa amani imerejea.


Kadhalika, Waziri Nchemba amesema katika kipindi cha 2016/17, Tanzania imewapa uraia wakimbizi wa Burundi 1,060 akaongeza kwamba
kati ya wakimbizi 247,000 waliopo nchini, 5,000 wameomba kurudi kwao.

 

=============

YALIYOJIRI KWENYE MKUTANO HUO

 

NGARA: Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza amewasili uwanja wa mpira wa Lemela, Ngara, Kagera na kupokewa na Rais Magufuli asubuhi hii.

Rais Magufuli amesema mazungumzo yake na Rais Nkurunziza yamehusu ushirikiano wa biashara na ujenzi wa reli kutoka Dar, Rwanda na Burundi.

NGARA: Rais Magufuli amemuagiza waziri wa mambo ya ndani kusitisha mara moja kutoa uraia wa Tanzania kwa wakimbizi wa Burundi na badala yake warudi kwao.

 

 

FUATILIA MKUTANO HUO HAPA

Leave a Comment