The House of Favourite Newspapers

Amber Lulu: Tunajichetua Kwa Ajili Ya Maisha

0
Msanii wa Bongo Amber Lulu akifanya yake na mpenzi wake.

MUUZA nyago maarufu kwenye video mbalimbali Bongo, ambaye kwa sasa amejitumbukiza kwenye muziki, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’, amefunguka kuwa vituko wanavyofanya hasa kwa kukaa nusu utupu ni kwa ajili ya kutafuta maisha na si vinginevyo.

                                     Amber Lulu akifanya yake.

Amber Lulu ameiambia Kilinge kuwa, mtu anaweza akamuona ni msichana mhuni au ana wanaume wengi, kitu ambacho siyo kweli, bali akifanya hivyo ni moja tu ya kusaka pesa kwa ajili ya kuendesha maisha yake ya kila siku na si kwamba ana tabia mbaya kama watu wanavyomchukulia.

 

“Jamani mfano mimi nikipiga picha nimevaa nguo ya ndani tu utakuta ni kwa ajili ya kutangaza nguo hiyo lakini siyo kwamba najinadi au kujiuza kwenye mitandao kama watu wanavyochukulia,” alisema Amber Lulu.

Leave A Reply