×

MSIBA WA NDIKUMANA, MASTAA WAANZA KUMIMINIKA NYUMBANI KWA UWOYA (VIDEO)

Ndikumana Hamad enzi za uhai wake.

Wasanii mbalimbali wamejitokeza nyumbani kwa msanii wa filamu, Irene Uwoya kumpa pole za kufiwa na aliyekuwa mumewe, Ndikumana Hamad aliyefariki leo.

 

Mastaa hao wamekusanyika nyumbani kwake maeneo ya Sinza-Mori jijini Dar es Salaam ambapo miongoni mwa mastaa hao, ni Video Queen, Agness Gelard ‘ Masogange’ na wasanii wengine chipukizi.

Msanii wa filamu, Irene Uwoya akiwa na na Ndikumana Hamad enzi za uhai wake.

Masogange, mbali na kuwepo msibani hapo lakini alionekana kukwepa mapaparazi baada ya kuwaona wakifanya kazi yao.

 

Kwa upande wa familia, walipotakiwa kuzungumzia taratibu za msiba huo, walidai kuwa bado kwa sasa hawawezi kuzungumzia chochote labda hadi hapo baadaye.

Leave a Comment