MVUA zinazoendelea kunyesha nchini zimesababisha kuharibika kwa daraja la miti la Kivule, sehemu za Kitunda jijini Dar es Salaam na kusababisha matatizo makubwa kwa wakazi wa sehemu hiyo.
Global TV Online iliyofika sehemu hiyo, imeshuhudia wananchi waliokuwa wanalitumia daraja hilo, wakivushwa kwa kutumia kivuko kilichotengenezwa kwa miti na madumu, ambacho si salama sana kufanya shughuli hiyo.