The House of Favourite Newspapers

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA HOSPITALI YA CCBRT JIJINI DAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mtoto Luke Maulid mwenye umri wa miaka 4 kutoka Mtwara ambaye anapata matibabu ya mguu katika hospitali ya CCBRT. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Bibi Helena Mjinja mwenye umri wa miaka 64 kutoka Musoma anayepata matibabu ya Fistula katika hospitali ya CCBRT jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanawake ambao wamepata matibabu ya Fistula na kupona na kisha kufundishwa kazi za mikono katika hospitali ya CCBRT jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Hospitali ya CCBRT Bw.Erwin Telemans juu ya utengenezaji wa viungo bandia vinavyotengenezwa kwa utaalamu wa hali ya juu.
Baadhi ya watoto wanaopata matibabu katika hospitali hiyo wakicheza mbele ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo juu ya utengenezwaji wa macho bandia kutoka kwa Mtaalamu wa Macho wa Hospitali ya CCBRT Bi. Rehema S. Semindu.
Akiendelea kutembelea wagonjwa hospitalini hapo.

Comments are closed.