×

BENKI YA NIC YAFUTURISHA WATEJA WAKE

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya NIC, Mick Karima (kushoto) akichukua futari.
Taswira ilivyoonekana katika hafla hiyo ndani ya Hoteli ya Hyatt Regency.
Futari ikiendelea kuchukuliwa.
Meneja wa idara ya wateja wadogo na taasisi wa benki ya NIC, Natasha Cathles (wa kwanza kulia) akiwa na baadhi ya wageni waalikwa.

 BENKI ya NIC  imewafuturisha baadhi ya wateja wake wa jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuboresha uhusiano na wateja.

 

Meneja wa idara ya wateja wadogo na taasisi wa benki hiyo,  Natasha Cathles, akizungumza kwenye hafla hiyo iliyofanyika hoteli ya Hyatt Regency alisema  anawashukuru wateja wa benki hiyo kote nchini  kwa kuendelea kuiamini benki yao katika kupata bidhaa na huduma za kibenki zilizo bora.

 

Lengo la futari hiyo  ni kukutana na wateja na kujadiliana jinsi ya  kuboresha huduma zao.

 

“Siku ya leo ni muhimu kwetu hapa Dar es Salaam kwa kuwa tunafuturu pamoja na kutakiana mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani  ambao unaendelea.

 

“Sisi kama Benki ya NIC,  tunawatakia mfungo mwema wa Ramadhani lakini pia maandalizi mema ya sikukuu!  Endeleeeni kufurahia huduma zetu mbalimbali na msiache kutembelea  matawi yetu yaliyopo nchini,” alisema Cathles.