×

SINGIDA MSHINDI WA TATU SPORTPESA SUPER CUP, YAIPIGA HOMEBOYZ 4-1

Timu ya Singida United imefanikiwa kushika nafasi ya tatu katika mashindano ya SportPesa Super Cup baada ya kutoka sare na baadaye kupiga mikwaju ya penalti ambapo Singida wameshinda 4-1 dhidi ya KK Homeboyz.

 

Kabla ya ushindi huo wa Singida, Kakamega Homeboyz ndiyo walikuwa wa kwanza kufunga bao kwenye mchezo huo lililofungwa na Opondo kabla ya Danny Lyanga kusawazisha kwa Singida United.

Mshambuliaji wa Singida, Danny Laynga (katikati) akiwatoka mabeki wa KK HomeBoyz wakati pambano hilo likiendelea.
Mabeki wa KK HomeBoyz wakimkaba Dues Kaseke wa Singida United aliye kati.

PICHA: MUSA MATEJA, NAKULU KENYA