
JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) wamewakamata watu saba katika hifadhi ya Saadan ambao wakiwa wanamiliki silaha ambazo walikuwa wakizitumia kufanyia uwindaji haramu katika hifadhi hiyo bila ya kuwa na kibali huku wakituhumiwa kumuua myama mmoja adimu anayepatikana kwenye hifadhi hiyo ya Saadan pekee aliyemtaja kwa jina Pongwe
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Jonathan Shanna amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Hadija Rashid ( 32 )mkazi wa Mkange amekamatwa na Magobore mawili, Amina Athumani (30) mkazi wa Gama amekamatwa na risasi tisa za Short Gun , Mohamed Athuman (65) mkazi wa Manda ambaye amekamatwa magobore mawili Yusuph Salum( 62) ,pamoja na Salum Ramadhan( 96)mkazi wa Manda amekamatwa na magobore mawili.
Kamanda Shanna amewataja watuhumiwa wengine kuwa ni Athumani Abdully (26), Siwatu Bakari(40) na Mussa Abdully wote wakazi wa Manda na walipokamatwa kila mmoja alikiwa na gobore moja.
Kufuatia tukio hilo Kamanda Shanna ametoa siku moja kwa raia wanaomiliki silaha isivyo halali kuzisalimisha mara moja.
Katika tukio la pili Jeshi la Polisi Mkoani hapa wamekamata gari lilikokuwa limeibiwa katika eneo la vigwaza mapema mwaka huu lenye namba za usajili T.265 BZCaina ya Mitsubish Canter tukio hilo lilitokea baada ya kundi la watu sita huku mmoja wao akijifanya ni mwalimu wa shule ya sekondari Vigwaza akiwa na wenzake walimfuata dereva aitwaye Omari Nyange(39) na kumwambia kwamba wanataka kumkodi ili wakahamishe vyombo dereva huyo alikubaliana na watu hao na walipoanza safari ya kwenda eneo la Madafu walimbadilikia na kumkaba kisha kumpora gari hilo na yeye kumtupa nje.
Baada ya taarifa hizo kufika katika Jeshi la Polisiwalianza upelelezi na Juni 6 mwaha huu wakalikamata katika Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro baada ya mwizi mmoja kukamatwa aliyetajwa kwa jina la Kasimu Nasoro(40) ambaye amekiri kuhusika na tukio hilo na kusema kuwa baada ya kuiba gari hilo walilibadilisha namba na kufunga namba za bandia ambazo ni T.525ABM na kulisafitisha hadi Mangula ambako walitengeneza kadi bandia na kwenda kuliuza kwa kiasi cha Sh. 8,000,000 kwa Florida Stanslaus mkazi wa Mang’ula Morogoro.
Katika tukio la tatu Jeshi la Polisi katika mzani wa Msata Wilaya ya Kipolisi Chalinze wamekamata madumu matupu ambayo yanadaiwa kukamata gari aina ya fuso lililokuwa linaendeshwa na dereva likiwa limebeba vyuma chakavu ambavyo havikulipiwa ushuru wa serikali ambapo walitozwa faini kiasi cha Sh. Mil. 2,000,000 na Maofisa wa kuhifadhi na kutunza mazingira kwa kosa la kukwepa ushuru.
Imeandaliwa na Khadijja Kalili Pwani.