
UBISHI wa kimichezo wa kuwekeana dau umezuka baina ya nyota wa soka wa Uingereza (England), David Beckham (aliyestaafu) na Zlatan Ibrahimovic wa Sweden anayeendelea kukipiga.
Malumbano yao yanahusu mpambano wa leo wa Kombe la Dunia baina ya nchi hizo mbili ambao utafanyika leo nchini Urusi. Beckham amemwambia Ibrahimovic atamnunulia samani (fanicha) kutoka kampuni maarufu nchini mwake (Sweden) kwa kuuza zana hizo ambayo inaitwa Ikea
Katika ujumbe alioutuma kwenye mtandao wa kijamii, Beckham amekubali ubashiri huo lakini amesisitiza Ibrahimovic lazima ahudhurie mchezo wa soka utakaopigwa katika uwanja wa Wembley (England) akiwa amevaa jezi la timu ya Uingereza iwapo timu hiyo inayoongozwa na Gareth Southgate itashinda.
Beckham ni mchezaji wa zamani wa timu ya LA Galaxy ya Marekani ambayo Ibrahimovic amejiunga nayo mwezi Machi mwaka huu.
Hivi ndivyo ‘viapo’ vya nyota hao wa soka walivyoweka katika mtandao

