
BAADA ya hivi karibuni msanii wa filamu, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ kufunguka kuwa ana mpango wa kubeba mimba ya mwanaume mwingine ili ndoa yake ya kanisani ivunjike rasmi, aliyekuwa mume wake kisha wakatengana, Michael Sangu ‘Mike’ ameibuka na kumpa ruhusa mwanamama huyo kuolewa au kuzaa hata na wanaume kumi.
Mike aliiambia Za Motomoto News kuwa, Thea ana uhuru hata wa kuolewa au kuzaa na mwanaume yeyote anayemtaka kwani yuko huru hakuna sheria yoyote inayombana kwa kuwa wakati wanafunga ndoa katika Kanisa Katoliki, walifunga ya mseto hivyo muigizaji huyo akawa anaendelea kusali kwenye kanisa la kilokole alikokuwa tangu mwanzo.
“Thea yuko huru kuolewa au kuzaa hata na wanaume kumi maana hakuna kinachomzuia, shida iko kwangu maana dini ya Katoliki inatambua ndoa moja tu ambayo nilifunga naye na hatujawahi kuibatilisha,” alisema Mike ambaye pia ni msanii wa filamu Bong
Stori : Mwandishi wetu.