×

Eric Shigongo: Mungu Amefanya!

KUFUATIA kifo cha mama yake mzazi, Bi. Asteria Kapera aliyeaga dunia alfajiri ya leo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete Muhimbili alikokuwa akitibiwa, mtoto wa marehemu, Eric Shigongo amesema neno hili kwa mama yake na waliomuuguza.

 

“Mungu amefanya! Baada ya kuugua kwa muda mrefu, leo, Mungu ameamua kumpumzisha mama yangu ambaye alinilea katika misingi ya dini, kuwapenda wengine na hata kujitoa kwa ajili ya wale wasiojiweza.

 

“Mama amefariki akiwa amenijenga, amenifanya nijione mimi ni wa thamani sana katika dunia hii. Ameondoka, Mungu amefanya, ninachoamini Mungu huwa hakosei, huwa anafanya mambo yake kwa wakati ulio sahihi kabisa.

 

“Inawezekana ningemwambia azuie hili basi kuna baya zaidi lingekuja. Mama alinifundisha kuhusu kupambana, leo ameona matunda ya kile ambacho amekuwa akinifundisha tangu utoto wangu.

 

“Sina cha kumshukuru bali ninamtakia maisha mema huko alipokwenda. Asanteni wote ambao mlikuwa nami bega kwa bega, shukrani kwa madaktari wa hospitali zote, Agha Khan, Muhimbili na nyinginezo kwa kujitoa kwa ajili ya mama yangu, namshukuru kila mmoja ambaye alijitoa kwa namna moja ama nyingine. Mungu awabariki sana.”

Eric Shigongo.

TANZIA: Mama Mzazi wa Eric Shigongo Afariki Dunia