×

Abdi Banda Afunga Ndoa na Dada wa Alikiba

Mchezaji anayekipiga klabu ya Baroka FC ya Afrika Kusini na timu ya taifa ya Tanzania,  Abdi Banda, akiwa na mke wake, Zabibu Kiba, baada ya kufunga ndoa.

MCHEZAJI wa timu ya Baroka FC ya Afrika Kusini na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na aliyewahi kuzichezea Simba SC ya Dar es Salaam  na Coastal Union ya Tanga, Abdi Banda, alfajiri ya leo Agosti 1, 2018 amefunga ndoa na Zabibu Kiba, ambaye ni dada wa mkali wa Bongo Fleva Ali Kiba kwenye msikiti wa Ahmad al maseeid uliopo Tabata jijini Dar es Salaam.

Mkali wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba ‘King Kiba’ (kulia),  akiwa na Abdi Banda na mke wake Zabibu Kiba.
Alikiba akimpongeza Abdi Banda baada ya kufunga ndoa.