HALI ya Waziri wa Maliasili na Utali, Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla imeendelea kuimarika vizuri kutokana na matibabu anayopatiwa katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alikolazwa baada ya kupata ajali ya gari akiwa mkoani Arusha kuelekea Dodoma kikazi.
Picha zilizotufikia zinaonesha Kigwangalla akiwa amepata nafuu na kutoka nje ya Jengo la Hospitali hiyo jambo linaloonyesha faraja huenda akapona hivi karibuni.
Mbunge huyo wa Nzega (CCM) alipata ajali wiki chache zilizopita baada ya gari lake kupinduka na kusababisha kifo cha Afisa habari wake, Hamza Temba aliyezikwa mkoani Tanga.
Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.
Comments are closed.