×

Makonda Aridhishwa na Ujenzi wa Barabara za jiji Lake

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, (wa nne kutoka kulia) akiangalia baadhi ya miundumbinu zinazojengwa katika jiji lake. Pembeni yake ni viongozi mbalimbali wa mkoa wake.
Mafundi ujenzi wakiwa kazini kuhakikisha wanajenga kwa wakati  miundumbinu hiyo.
Daraja la watembea kwa miguu eneo la Lugalo Da, ujenzi ulipofikia  kama linavyoonekana. 
Ujenzi ukiendelea eneo la  barabara ya Wazo hadi Goba.
Mafundi ujenzi wakiwa kazini.

 

Mkuu wa Mkoa wa  Dar es Salaam, Paul Makonda, leo ametembelea miradi mbalimbali ya ujenzi wa barabara zinazojengwa katika jiji lake na  kuridhishwa na ujenzi  huo inayojengwa chini ya  Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADs) inayogharimu  zaidi ya Bilioni 24.

 

 

Akizungumza wakati wa  ziara yake ya kukagua ujenzi huo, Makonda, amesema  hatua iliyofikiwa inaridhisha.

Katika ziara hiyo  Makonda amekagua barabara ya Wazo hadi Mbenzi Luis, Goba hadi Mbezi Masana ambapo   ujenzi wake ni wa kiwango cha lami.

 

 

Aidha Makonda amesema ujenzi wa daraja la kivuko cha watembea kwa miguu  katika barabara ya Bagamoyo eneo la Lugalo  uko katika hatua za mwisho na  umegharimu zaidi ya Bilioni  1.

 

 

Makonda amesema, kukamilika kwa barabara hizo kutafungua fursa kwa wananchi na kuwezesha  maendeleo katika maeneo hayo. Pia ameeleza kuwa  huo ni utekelezaji  wa  ahadi ya serikali ya awamu ya tano  chini ya Rais Dk. John Magufuli.