×

NMB Yatoa Vifaa Vya Michezo Kwa Jeshi la Wananchi Tanzania

Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo na Kati wa Benki ya NMB, Salie Mlay akimkabidhi baadhi vifaa vya michezo Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanda ya Ngome, Kanali Damian Majare. Kulia ni Mkurugenzi wa Utimamu wa Mwili, Michezo na Utamaduni wa JWTZ, Kanali Erasmus Bwegoge.

 

BENKI ya NMB imetoa vifaa vya michezo kwa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya mashindano ya majeshi yanayotarajia kufanyika Aprili, mwakani.

Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo na Kati wa NMB, Salie Mlay amesema vifaa walivyokabidhi kwa JWTZ vina thamani Sh milioni 12.5.

“Vifaa hivyo ni kwa ajili ya timu mbalimbali za JWTZ kwa michezo ya soka, netiboli na kikapu ambavyo thamani yake ni Sh milioni 12.5. Timu hizo zinatarajiwa kushiriki mashindano ya majeshi ambayo yatafanyika mwakani,” alisema Mlay.