
WAPENZI wa burudani usiku wa kuamkia leo wamepata burudani ya aina yake katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar wakati Tamasha la Fiesta lililosheheni mastaa kibao lilitoa burudani ya kufa mtu.

Awali tamasha hili lilitarajiwa kufanyika Novemba 24, mwaka huu kwenye Viwanja vya Leaders, Dar, lakini lilisitishwa kutokana na sababu mbalimbali.

Mastaa waliopanda kwenye jukwaani ni AliKiba na kundi lake, Kundi la Nako 2 Nako likiongozwa na Joh Makini na wenzake, Juma Nature, Fid Q, Chege, Mr Blue, TID, Vanessa Mdee, Rich Mavoko, Msami, Maua Sama, The Mafik, Christian Bella, Rosa Ree na wengine wengi.


PICHA: RICHARD BUKOS | GPL
Huyu MSAMI Sasa BASI! Afanya kufuru Stejini, FIESTA!
Cheki ROSTAM, MAUA SAMA Walivyo iokota FIESTA!