The House of Favourite Newspapers

Cardi B Avunja Rekodi Tuzo za Grammy Miaka ya 2000

RAPA wa kike, Belcalis Marlenis Almánzar, maarufu kama Cardi B amevunja rekodi ya kuwa mwanamuziki wa kike kupokea tuzo ya album bora ya rap kwa miaka ya elfu mbili, Februari 10  siku ya Jumapili katika ugawaji wa tuzo  61 za Grammy.

Katika kipengele hicho alikuwa anashindana na wasanii wakali katika game akiwemo, Pusha-T, Macmiller, Nipsey Hussle na Travis Scott .

Baada ya kupokea tuzo hiyo aliwashukuru wote  waliohusika kutengeneza album yake kwa kuchangia hata mchango wa mawazo na washiriki ambao walikuwa kwenye kipengele kimoja kugombea naye tuzo.

Mwanadada Lauren Hill ndiye wa mwisho kunyakua tuzo ya kundi  kwa album bora ya rap, ‘The Core’  mwaka 1995.

Baadhi ya marapa wa kike akiwemo Lil Kim  na Remy Ma walitpa pongezi  kupitia akaunti zao za tweeter.

 

JIUNGE NA FAMILIA YA GLOBAL TV UPANDE MTANDAO WA MAFANIKIO

Bofya hapa kujiunga na familia ya Global TV Club ==> Global TV Family Club

Comments are closed.