×

JPM APOKEA DHAHABU, FEDHA ZILIZOKAMATWA KENYA (PICHA +VIDEO)

Rais  John  Magufuli akisaidia kuhesabu vipande vya dhahabu huku akishuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi (wa pili kulia) aliyevipokea kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Balozi Monica Juma (wa kwanza kushoto).   Dhahabu  na pesa hizo vilikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi vikitoroshwa kutoka Tanzania.  Hafla hiyo ya makabidhiano ilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo Jumanne,  Julai 24, 2019.

 

RAIS John Magufuli leo Jumatano,  Julai 24, 2019,  ameshuhudia makabidhiano ya dhahabu iliyokamatwa nchini Kenya iliyowasilishwa na mjumbe maalum wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Monica Juma.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

 

Akizungumza katika makabidhianayo hayo, Waziri Juma alisema:

“Tunashukuru kwa kumpokea rais wetu kule Chato. Tulipokutana Entebbe  mlituamrisha kuwa tusipofanya haraka mtajipangia kukutana, tulipopata  simu, nikamuuliza rais nitakuja Chato?  Akaniambia ‘huwezi, nitakwenda  mwenyewe’ kwa kuwa nyie hamkupanga.

 

“Leo tuna furaha sana, nilikuwa kwa muda mrefu nikitamani kufika Dar.  Tumefika hapa leo kuleta ujumbe kutoka kwa ndugu yako Rais Kenyatta.  Amenituma kukuletea wewe ujumbe na pia dada na kaka zetu wa Tanzania kupitia wewe.”

 

Profesa  Kabudi akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Monica Juma. 

Naye Rais Magufuli  baada ya kushudia makabidhiano ya dhahabu amesema:

“Namshukuru Rais Kenyatta kwa upendo na uaminifu mkubwa alionao kwa kurejesha dhahabu yenye uzito wa kilo 35 pamoja na fedha, Rais Uhuru amefanya kitendo cha kiungwana kwa kuturudishia madini yetu ambayo yalikuwa yametoroshwa.

“Navipongeza vyombo vya ulinzi na usalama vya Kenya kwa kazi kubwa walioifanya.

Rais Magufuli akimshukuru Waziri Juma baada ya makabidhiano.

“Tuliamua kuchukua hatua za makusudi za kuweka mikakati ya kulinda rasilimali zetu za madini ili ziweze kuwanufaisha Watanzania.

“Wa kupongezwa kwa hili ni vyombo vya Kenya, najua wakuu wa vyombo hivyo Tanzania mpo hapa, lazima niwatandike kwa sababu vitu vimetoka Mwanza vimekamatiwa Kenya.  Je,  vilipobebwa Mwanza na Kilimanjaro vyombo vyetu vilikuwa vinafanya nini?

…Akimsikiliza Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan,  akisalimiana kwa simu na Rais wa Jamhuri ya Kenya,  Jomo Kenyatta,  baada ya viongozi hao kushuhudia makabidhiano.

‘Vitu vya fedha na dhahabu vinahitaji moyo wa jiwe, kiukweli Rais Kenyatta ni muaminifu, kwani vingeweza kupigwa, lakini fedha hizi zimerudi Tanzania baada ya miaka 15.  Lakini na mimi mnipongeze, inawezekana wengine wangepiga dili juu kwa juu na wala msingejua.

“Mali za wananchi lazima zirudi kwa wananchi kwa ajili ya maendeleo, Kenya na Tanzania ni kitu kimoja.”

Pia Magufuli alisema Kenya imeahidi kununua unga kutoka Tanzania badala ya mahindi, jambo ambalo alisema ndiyo udugu na urafiki wa kweli.

…Akiongea baada ya makabidhiano.