×

Vilio! Kitongoji Chafutwa, Wakazi Hawana Pa Kuishi Wala Kupigia Kura! – Video

Mwandishi wa habari, Lucas Masungwa (wa pili kushoto) akichukua taarifa kwa baadhi ya wananchi wa Kitongoji Cha Razaba Wilaya ya Bagamoyo kuhusiana na mgogoro uliopo juu ya kutakiwa kuondoka katika kata hiyo.
Baadhi ya wakazi wa Kitongoji Cha Razaba wakitafakari kujua hatma yao na Serikali kuwaondoa katika kata hiyo. Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kijiji cha Matumbini, Ally Mussa Kitunguu.
… Masungwa (aliyepo katikati) akiendelea kuchukua taarifa kwa baadhi ya wananchi wa Kitongoji Cha Razaba.

 

WAKAZI wa Kitongoji Cha Razaba Wilayani Bagamoyo Wameelezea masikitiko yao juu ya kufutwa kwa kitongoji hicho na uongozi wa serikali ya Wilaya jambo linalodaiwa kuwanyima haki ya kujiandikisha na kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24, mwaka huu.

 

Global TV Online imefika eneo hilo na kuzungumza na baadhi ya wawakilishi wa wananchi na viongozi wa ngazi za kijiji ambao walielezea masikitiko yao na kumwomba Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuingilia kati ili kuwanusuru na janga la kukosa makazi linalowakabili.

 

Wakazi hao walisema kuwa, wamezaa watoto na baadhi yao tayari walikwisha oa na kuolewa wakiwa eneo hilo hivyo wanashangaa kupatiwa taarifa ya mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo  kuwataka kuondoka pasipokujua waende wapi. Kilio chao wakakielekeza kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili aweze kutatua mgogoro uliopo kwenye eneo hilo, licha yao wao kudai kwamba kama ni eneo la serikali basi waoneshwe eno lingine la kwenda.

 

Aidha, Global TV Online kutaka kujua ukweli wa madai hayo  ulizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainabu Kawawa ambaye alifunguka haya.